2016-12-12 16:54:00

Papa Francisko acheni vita, amani itawale!


Papa Francisko wakati wa Sala ya Malaika wa Bwana, Jumapili tarehe 11 Desemba 2016 alikumbuka mashambulizi ya kigahidi iliyotokea Jumapili  11 Desemba, 2016 katika maeneo tofauti huko Cairo Misri ambapo mashambulizi yalifanyika  katika Kanisa , Kanisa kuu la kikopti la mtakatifu Marko na kusababisha vifo vya watu na majeruhi, akisema ”Ni sehemu nyingi ambazo kwa bahati mbaya  ni ghasia zinasababisha machafuko na kuleta vifo na uharibifu.

Jibu moja katika matatizo hayo ni Imani kwa Mungu, umoja katika maadili ya kibinadamu pamoja na ustaarabu. Aidha alitoa salam zake kwa watu wote na pia   kuonyesha mshikamano na ukaribu kwa Papa Tawadros II na Jumuiya yake ya kikristo kutokana na shambulizi la Kanisa Kuu la Kikoptik na kusali kwa ajili ya wote waliopoteza maisha na majeruhi. Kufuatia na habari za shambulio la kigaidi  huko  Cairo inasadikiwa watu 25 kufa na hasa ni watoto na wanawake kwasababu wataalam wanasema bomu liliangukia sehemu inayokaliwa na wanawake wakati wa kusali  ndani ya Kanisa Kuu la Mtaktifu Marko makao Makuu ya Patriaki wa kikopta Papa Tawadros II.


Naye waziri wa mambo ya ndani ya nchi Magdi Abdel- Ghaffar akikaririwa na Gazeti la Asia , linasema walitembelea sehemu zote zilizoharibika, na kuona  vipande vipande vya madirisha ,na  damu zilizokuwa zimatawanyika kila upande. Aidha wanasema Shambulio la Jumapili ni mojawapo ya mashambulizi mazito  yalitokea katika Jumuiya ya wakristo wa Kikopta. Mara ya mwisho ilikuwa shambulizi ni lile la Januari 2011 huko Alessandria lililosababisha watu 21 kupoteza maisha yao na 70 kujeruhia.


Aidha Papa aliwakumbuka waliotangazwa kuwa wenye heri, ni wafiadini 17 walio uwawa huko Laos kati ya 1954 na 1970 na wanajeshi wa kikomunisti  wa Patthet Lao, na kutangazwa na Kanisa kuwa wenye heri  Jumapili 11 Desemba  huko Vientiane mji wa nchi huko kusini mwa Bara la  Asia . Kati yao kuna mmisionari mmoja Mario Borzaga kutoka nchini Italia na wenzake 14 waliouwawa kutokana na kutetea imani yao   wa Shirika la  kimisionari oblati wa Maria mkingiwa wa Asili .


Hivyo baba mataktifu alisema  huo ni ujasiri na kuwatia moyo, uwe mfano kwa wamisionari  hasa hasa kwa makatekista katika sehemu za kimisionari ambao kazi yao ni tunu msingi ambayo siyo rahisi kuoindoa, na Kanisa linawashukuru kwa mchango wao , aliendelea ” Makatekista wanafanya kazi nzuri tuwapigie makofi hao wanao peleka ujumbe wa Bwana ili upate kukua ndani mwetu.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.