2016-12-06 15:54:00

Jumuiya ya Kimataifa inadhihirisha maadili na wajibu, ili kukuza hali ya kuaminiana


"Katika kukuza usalama wa nyuklia, Jumuiya ya Kimataifa inadhihirisha maadili na wajibu, ili kukuza hali ya kuaminiana na kuimarisha usalama, vyama vya ushirika kwa njia ya mazungumzo ya kimataifa" ni maelezo katika ujumbe wa  Monsinyo Antoine Camilleri, Msaidizi wa Katibu kwa Mahusiano na nchi za nje Vatican  akizungumza katika  Mkutano wa pili wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia  huko Vienna Austria mwezi huu.
Katika jumbe wake Monsinyo  anaelezea juu ya mantiki ya hofu na kutokuaminiana katika kuzuia   nyuklia, alisema lazima  kubadili mantiki mpya ya maadili ya kimataifa .Tunahitaji maadili ya uwajibikaji , mshikamano na ushirikiano wa usalama wa kutosha na kazi ya kuweka chini  uthibi wa nguvu katika  teknolojia ya nyuklia.


Kwa mujibu wa Monsinyo Camilleri anasema, vitisho kwa usalama wa nyuklia ni changamoto kubwa kitaalam na kidplomasia na kwa kujibu hilo ni muhimu kushughulikia miendendo mipana  ya Usalaman siasa , uchumi, utamaduni ambayo uongoza hali  na mashirika yasiyo ya kiserikali katika kutafuta usalama , uhalali  au nguvu katika silaha za nyuklia.


Vatican inaona umuhimu wa mkubwa kwa kuendeleza usalama wa nyuklia , kwa madhumuni ya kuimarisha utawala na wala siyo kuenea kwa upungufu wa silaha za kinyuklia, hata kwa ajili ya kukuza teknolojia ya nyuklia kwa malengo ya amani. Aidha Monsinyo anaonyesha sehemu mbili zinazotakiwa  kuongeza juhudi , ya kwanza ni ulinzi wa kimwili na wa nyenzo za kinyuklia , kwani kushindwa kudhibiti kunaweza kuleta  athari  mbaya; pili sehemu nyingine anaonyesha umuhimu wa kulinganisha vitisho vya ndani na kuzuia mashambulizi dhidi ya data na miundo nyeti, ambapo inabidi   kuongezeka ulinzi kuanzia ngazi za usalama wa habari na kompyuta, kwa kuhifadhi siri za taarifa muhimu kwa usalama wa nyuklia

.
Msaidi wa Katibu kwa Mahusiano na Nchi  Monsinyo Camillieri alibainisha pia mafaniko makubwa yaliyopatika katika kuimarisha usalama wa nyuklia , na kuwashukuru Shirika la Kimataifa la Nishati na Nyuklia kwa juhudi zao kwa ppindindi chote cha miaka hii , wakati huo huo alilisistiza kwamba sehemu kubwa ya mafaniko ya Shirika la  Kimataifa la  Nishati linategemea dhamira ya nchi wanachama kufikia ahadi zao za kisheria na kimaadili, na kusema “ majukumu ya nchi wanachama lazima kubaki na lengo la mjadala wetu wetu”.


Na mwisho wa hotuba yake alimazia  mwakilishi wa Vatika huko Vienna akiweka wazi kwamba  haiwezekani kufanya ndoto kuhusu uzito wa changamoto zinazokabili jumuiya ya kimataifa , lakini kwasababu ya changamoto hizi  Vatican  inakubali kuunga mkono kwa msaada kwaajili Shirika hilo.
Mkutano katika  kupiga marufuki silaha za nyuklia unakwenda sambamaba na ujumbe wa baba Mtakatifu Francis alipotembelea katika Baraza la Umoja wa Mataifa mwaka 2015 akiwataka kutafuta njia ya kufanya ili dunia isiwe na  silaha za kinyuklia na kupiga marufuku kiujumla hayo mabomu.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.