2016-10-11 14:54:00

Ujumbe wa Maaskofu Ulaya waonya Kukana Mungu ni kudhoofika kiroho na kijamii


Kumkana  Mungu au kukataa kumwamini  Yesu Kristo,  si uhakika wa  mtu kusonga mbele kimaendeleo, bali huwa  chanzo cha umaskini wa kiroho na kimaadili, ambao umekuwa ni sifa ya Ulaya kwa nyakati zetu. Na ikiendelea kwa muda mrefu, hutengeneza utamaduni wa umaskini miongoni mwa jamii si kiroho tu lakini hata  kiuchumi pia.  Ni ujumbe kutoka Mkutano wa kwanza wa Baraza la  Marais wa Mabaraza ya Maaskofu wa Ulaya. Ujumbe huo umeelekezwa kwa  wakazi wote wa Ulaya, ambamo kwa wakati huu kuna mwelekeo wa kutaka kutelekeza Ukristo kwa kishindo kikubwa.  Marais wa Mabaraza ya Maaskofu Katoliki wa Ulaya, walitoa onyo hili wakati wa mkutano wao uliofanyika huko Monaco . Mwisho wa Mkutano  huo, Maaskofu walimchagua  Rais Mpya , chini ya Usimamizi wa Kardinali Angelo Bagnasco.  

Maaskofu wamesema, pale dini inapotumiwa katika uhalisi wake , huwa na nguvu za kukuza vizuri ubinadamu na maendeleo shirikishi.   Kwa  mtazamo huo, Maaskofu wameonyesha  matumaini yao kwamba,  barani Ulaya, ambapo kwa wakati huu mna ishara nyingi za  kuweka   pembezoni  majukumu ya  Kikristo,  kupitia vitendo vya kibaguzi,  kwa fikira kwamba , malimwengu ndiyo yenye kuifanikisha jamii , hizi ni fikira potovu. Ni muhimu kwa jamii ya Ulaya kutambua maana na thamani halisi ya dini katika jamii na katika maisha ya mtu binafsi na jamii kwa ujumla..

Katika mkutano huu wa kwanza wa mwaka , Maaskofu pia walizungumzia dharura ya kupata jawabu kwa ongezeko la matukio mengi yanayoleta mateso makubwa kwa Wakristo,  sehemu mbalimbali za dunia.  Maaskofu wametoa tamko lao kali lenye kulaaani matukio yote yanayoathiri  haki za binadamu na uhuru wake na hasa haki kwa dini. Maaskofu wamelaani  dalili zozote zile zinazchochea moto wa vurugu na madhulumu yanayomotishwa na sababu za kidini wakisema huu ni  unyanyasaji na ukiukwaji wa  matumizi ya jina la Mungu.

Kwa maoni hayo Maaskofu wametoa ombi lao kwa setrikali zote duniani , zikatae katakata matumizi ya ghasia na dhuluma kama njia ya kueneza dini , kama ambavyo kwa mara nyingi  Papa Francis, amelalamikia matumizi ya jina la Mungu , kufanya fujo na ukatili , akisema huku ni kukana haki za binadamu na Mungu pia . Wamesema , wao wakiwa Maaskofu katika  mkutano huu wa Monaco, wakiongozwa na wasiwasi wanaouona kupitia kazi zao za kichungaji, wanatoa wito kwa wahusika na kuwaongoza watu , kiserikali au kimamlaka kitaifa au mataifa, , kufanya kazi  ya ziada ili kuhakikisha heshima na uadilifu wa watu binafsi na jamii unarejeshwa kama ilivyokuwa katiak miaka yanyuma, na  hasa  kwa wale amba sasa wanaishi katika mazingira magumu zaidi.Ujum be wa Maaskofu hasa unaelekeza mawazo kwa Wakaristo wahamiaji na wale wanoteseka kwa sababu ya imani yao. 








All the contents on this site are copyrighted ©.