2016-09-05 09:37:00

Ni lazima kujiuliza Mungu anataka niishi vipi katika maisha yangu?


Kumfuatia Yesu ni kazi kubwa. Lakini wakati huohuo kwa wanaomfuata hujazwa na furaha kubwa ,hupata  ufahamu na ujasiri wa kumtambua  Mungu katika watu maskini wa maskini na hivyo  hujitolea  kwa moyo wote na kujenga  urafiki na maskini na kuwahudumia kwa ukarimu.  Baba Mtakatifu Francisko ameeleza hayo ,katika  homilia yake,  wakati wa Ibada , aliyoiongoza katika  uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakaifu Petro , Jumapili  illiyopita , 04 .09.2016, kwa nia ya kumtangaza kuwa Mtakatifu , Mama Mpendwa Tereza wa Calcutta, Mama wa maskini.   Papa aliomba  ushuhuda wa Mama Tereza wa kuishi kwa kumtegemea Mungu , na uendelee kuwaleta wote hasa maskini wa maskini karibu na Mungu.

Papa katika homilia yake, akiyatazama maisha ya Mtakatifu Mama Tereza, na watu wengine wanaojitolea kuhudumu wengine bila kudai malipo, alisema utendaji a watu hawa ,  ni  upendo wa Yesu, wenye kuwapa  msukumo kutoka ndani ya moyo,  kwenda  kutumikia maskini na wahitaji, bila kutarajia shukrani yoyote au malipo, badala yake wanaonekana kujikatalia yote , kwa sababu wameugundua upendo wa kweli.

Aliendelea kusema, faraja yao ni kuinamia mtu maskini na mhitaji, kama ilivyo kwa Bwana wao ambaye alikuja duniani na kujishusha  chini, akiwainamia  wote hasa wale waliopoteza imani  na wale wanaoishi kama  kwamba Mungu hayupo.  Papa alisisitiza kuwa Yesu anawainamia wote,  hasa vijana waliopoteza  maadili , familia zilizo katika kipeo cha maisha , wagonjwa wote , wafungwa, wakimbizi na wahamaiji ,  na wanyonge  wasioweza kujitetea wenyewe kimwili na kiroho pia , watoto waliotelekezwa na wazee walioachwa wenyewe. Yesu yuko kila mahali ambako mtu anatafuta msaada ili apate kuinuka.

Papa alitaja kwa hao , hapo ndipo  uwepo  wa mfuasi wa Kristo  na  Kanisa unatakiwa kuwepo , kutoa farija  na  matumaini mapya kama jambo la lazima kwa mfuasi wa Yeu na Kanisa .

 Homilia ya Papa ililenga katika masomo ya liturujia ya neno la siku,  somo la kwanza lilitoka  Kitabu cha Methali  (9;13 ). Kabla ya maelezo yake, Papa Francisko alihojii  "Nani anaweza kujifunza shauri la Mungu?".  Alitoa ufafanuzi kwamba, swali hili kutoka Kitabu cha  Methali,  linaonyesha  kwamba, maisha yetu ni Siri ya Mungu,  na kwamba hatuna ufunguo wa ufahamu  juu ya hilo, ila tunatambua kwamba,  katika maisha watendaji wakuu husika katika historia yote ya maisha  ni Mungu na mwanadamu. Na hivyo sisi  kama binadamu kazi yetu ni kuitikia kile Mungu anachotaka tutende katika maisha yetu. Ni  kufanya mapenzi yake.

Papa aliendelea kuhoji kwa namna gani tunaweza itikia kufanya mapenzi ya Mungu  katika maisha yetu? Alitoa jibu akisema,  kwanza zaidi ya yote ni lazima kujifunza yapi yanampendeza Mungu . Kuelewa  Mungu anataka nini, na haya tunaweza kujifunza kutoka katika maisha ya Manabii na watakatifu, Maisha yao  hutangaza  yale  yaliyompendeza Mungu.

Na kwamba,  kwa kifupi maisha yao hutoa jibu la kushangaza , lililoandikwa katika  Kitabu cha Hosea na Injili: "Nataka huruma, wala si sadaka" (Hos 6: 6; Mt 9:13). Kumbe  Mungu anaridhia  kila tendo la huruma, kwa sababu katika kusaiidia  watu wahitaji wake kwa waume ,  tunatambua uso wa Mungu ambao hakuna mtu anaweza kuona hivihivi tu  (cf. Yohana 1:18). Kila wakati tunapo  wainamia watu wahitaji na kutoa msaada wetu , iwe msaada wa chakula, kinywaji  au  mavazi ,tunakutana na  Yesu, tunamwona  Mwana wa Mungu (Mat 25:40).

Papa aliendelea kuzungumzia utendaji halisi , kama tunavyoomba katika sala na  kukiri hakuna mbadala wa upendo: wale ambao kwa riadhaa yao hupenda  kuwahudumia wengine ,wakati mwingi bila hata yakujua  hilo, watu hao  ni wale wanaompenda Mungu (cf. 1 Yohana 3: 16-18; Yak 2: 14-18).  Hayo nidiyo maisha ya kikristo, na si  tu kurefusha  mkono  wakati wa shida lakini daima , hupenda mshikamano na binadamu wengine bila kutafuta faida binafsi. Papa amesisitiza na kumtaka kila mwanafunzi wa Yesu anayaweka maisha yake katika utumishi wa  upendo kama wajibu na si kama ajira.

Papa alieleza na kuurejea umati mkubwa wa watu waliofika Rome kwa ajili ya maadhmisho ya Jubilee ya huruma , kwa wahudumu wa kujitolea, akisema wameonyesha upendo halisi na thabiti kwa Mwalimu wao kama ilivyoadikwa katika Injili ya Luka 14:25. Papa alieleza na kufanya rejea kwa maneno ya  Mtume Paulo: ”Ndugu upendo wake umeniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana. Nawe umeichagamsha mioyo ya watu wa Mungu  (Flm 1: 7)”.  Papa  hakuweza ficha furaha yake, hasa kwa jinsi walivyoweza  leta furaha na matumaini mapya kupitia kazi zao za kujitolea. Kwa jinsi  mikono yao inavyofanya  kazi ya kuwainua waliokata tamaa na kupagusa machozi ya wengi , kwa  jinsi walivyomwaga upendo wao  kwa unyenyekevu na bila kujihurumia katika huduma . Papa anasema , huduma yao yenye kustahili kusifiwa kwa kutoa  sauti ya  imani, na inaonyesha  huruma ya Baba, ambaye  huwakaribisha na kuwapokea wahitaji wote.

Papa kisha aliyarejea maisha ya Mama Teresa wa Calicutta akisema  katika nyanja zote za maisha yake, alihudumia kwa ukarimu mkubwa akionyesha  huruma ya Mungu,  yeye mwenyewe alikuwa tayari kumhudumia  kila mtu na hasa waliowekwa pembezoni  au kutelekezwa na jamii. Alikuwa n ni mtetezi wa maisha ya wote na bila kuchoka kutangaza kwamba "wasiozaliwa bado ni dhaifu , wadogo na wahitaji zaidi. Na aliwainamia wale waliokuwa katika hali za kufa , waliolala kando ya barabara ,bila msaada , lakini yeye aliwainamia na kwasaidia kwa kuwa aliiona sura yaMungu kwao. Alifanya sauti yake isikike hata mbele ya dunia yenye mamlaka , iweze kutambua  kuwa na hatia ya kutowahudumia umaskini.

 Mama Teresa, upendo na  huruma, ilikuwa ni "chumvi" iliyoweka  ladha katika  kazi zake, ilikuwa ni "mwanga" uliomulikia giza la wengi waliokata tamaa katika umaskini wao na mateso  yao. .

Papa Francisko alimalizia homilia yake akisema utendaji wa Mama Tereza hata leo hii ni ushuhuda fasaha muhimu sana katika kuwakaribia watu maskini walio  sahaulika katika mitaa ya miji.  Hivyo  Mama Kanisa  kwa a fadhila zake , linamweka wakfu na kumtangaza kuwa Mtakatifu , Mfano wa kuigwa na wote na hasa wanao huduma kwa kujitolea . Papa alimtangaza na kuomba msaada wake uweze  kuwa kioo cha upendo wa kuhudumia  bila kuchoka , katika kila hatua za itikadi na majukumu yote, kutenda kwa ukarimu na huruma kwa kila mtu bila ubaguzi wa lugha, utamaduni, rangi au dini., kama  Mama Teresa alivyopenda kusema, "siwezi  kuzungumza lugha yao, lakini naweza kutabasamu".  Kwa maneno hayo , Papa ametoa  mwaliko kwa wote kuwa na tabasamu ndani ya moyo  kwa ajili ya  kuwapa wale tunaokutana nao katika safari yetu ya maisha , na hasa wale wanakabiliwa na kukosa mahitaji ya lazima. Kwa namnahiyo tunafugua njia na fursa ya furaha na matumaini , kwa watu wengine wake kwa waume , kwa watu  wengi a waliokata tamaa ambao wanahaja ya kueleweka na kuhurumiwa ..

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.