2016-08-01 09:41:00

Siku ya Kimataifa ya Urafiki: Urafiki ni dhamana ya amani na utulivu kimaisha


Jumamosi iliyopita 30 Julai , ilikuwa ni  Siku ya Kimataifa ya Urafiki  kati ya watu ikienda sambamba na siku ya Kimataifa dhidi ya usafirishaji haramu wa watu .

Siku ya Kimataifa ya Urafiki ilitangazwa mwaka 2011 na Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa fikra kwamba,  urafiki kati ya watu, nchi, tamaduni na watu binafsi, unaweza hamasisha juhudi za amani na kujenga madaraja kati ya jamii.

 Azimio hilo namba  A / RES / 65/275) linaweka mkazo hasa juu ya kuwashirikisha vijana, kama viongozi wa baadaye, katika shughuli za jamii,  za tamaduni mbalimbali,   tangu ngazi za chini hadi kimataifa na kukuza na kuheshimu tofauti zao.   Siku pia nia ya kusaidia malengo na madhumuni ya Azimio na Mpango wa Utekelezaji juu ya Utamaduni wa Amani na kupinga Vurugu kwa Watoto wa Dunia.

Kwa adhimisho la mwaka huu  2016,   Katibu Mkuu wa Moja wa Mataifa Bwana Ban Ki moon,  ametoa ombi   kwa kila mtu, kuungana  katika roho ya pamoja ya mshikamano wa binadamu ili kuondokana na migogoro inayokabili  jamii.

Ban Ki moon ameutaja Urafiki  kuwa ndiyo furaha yenyewe ya maisha na  ustawi wa mtu. Urafiki ni dhamana inayowezesha kila mtu  kuchangia mageuzi makubwa ya haraka  yanayotakiwa kufikia utulivu kudumu duniani. Na ameomba  kupanua mikono katika urafiki na kujenga  mahusiano ya kuaminiana, ili jamii iweze kufuma  wavu wa usalama kwa ajili ya kuzishinda nguvu za makundi au majeshi yanayo jaribu kudhoofisha amani, usalama na maelewano ya kijamii.

Katibu Mkuu  ana  imani kwamba katika kuelewana na kufahamiana  zaidi, pia hujenga moyo wa huruma kwa wengine na sana walio katika hali ngumu za maisha. Maelewano na umoja huzaa  ulimwengu ulio bora  zaidi, kwa kuwa huwezesha  wote kushikamana katika umoja na  hivyo kutendea kwa wema zaidi.  Moyo wenye mapenzi ya kujenga urafiki na wengine hujinasua na itikadi za chuki na fitina na ukiukwaji wa haki za binadamu. Itikadi  kama hizo  kwa  namna fulani  huchukuliwa kama ni usaliti wa urithi wa ubinadamu na huweka hatarini  ustawi  wa wanadamu kwa  wakati ujao.

Usaliti kama huo aliendelea kusema Bwana Ban,  unaweza  kushindwa  tu kupitia njia ya  umoja  wenye  kukuza na kutetea roho ya  mshikamano  na umoja wa binadamu katika kupambana na mzizi unaoleta changamoto  katika maisha kama vile umaskini, vurugu na ukiukwaji wa haki za binadamu.

Roho hii ya mshikamano, Katibu Mkuu alisema, ni wazi inaweza onekana katika njia nyingi, tangu katika mfumo wa ngazi ya chini wa urafiki binafsi hadi kaika ngazi ya kimataifa.  Na alihitimisha ujumbe wake kwa ajili ya "Siku hii ya Kimataifa ya Urafiki” akitoa wito wa kutatua matatizo yaliyoko kwa  kufanya mageuzi  yenye kujenga uhusiano mzuri haraka iwezekanavyo, na  kuyarutubisha  maisha yetu wenyewe  kwa  amani  na utulivu,  kwa sasa na kwa ajili ya siku zijazo. 








All the contents on this site are copyrighted ©.