2016-07-25 10:12:00

Misri: Sheria zinahakikisha haki sawa katika utendaji kwa Watu wote


 Waislamu, Wakristo na serikali wanapaswa kuwa macho na jaribio lolote lile linalotaka kuitumbukiza jamii katika  mtego wa kutoelewana. Ni lazima Wamisri na watu wote kutambua kwamba, wale wote wanatakaobainika kuchochea au kuhusika na vurugu za kidini au mashambulizi, watakabiliwa na mashitaka na kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria kwa sababu "Misri inaongozwa kwa  utawala wa sheria.  Rais wa Misri Abdel Fattah al Sisi,  alieleza wakati akiitoa msimamo wake,  kuhusu vurugu za mapigano ya kikabila ya hivi karibuni  hasa katika wilaya ya Minya, ambako ghasia hizo zilisababisha Mkristo wa Kanisa la Kikoputiki kuuawa na wapiganaji wa  Kiislamu. Rais al Sisi alitoa onyo hilo wakati wa sherehe za kukabidhi vyeti wanajeshi. Katika khafla hiyo, alitoa wito wa maelewano  kati ya  dini na  makabila, akitaja pia dhamira yake ya kumfikisha mbele ya sheria mtu yeyote anayetaka kuzua machafuko au kuanzisha  vita kati dini.

Shirika la habari za Fides limetaarifu kwamba,Rais  Al-Sisi alitoa wito  kwa Wamisri wote kufanya kazi za  kukuza umoja wa kitaifa, huku akiwahakikishia kwamba,  sheria za Misri zinatambua kwamba, Wakristo na Waislamu wote ni sawa kisheria.

Nae Mkuu wa Kanisa Misri, Patriaki Tawadros II, baada ya mkutano mfupi na Rais al Sisi, aliuhutubia mkutano wa wanahabari  akisisitiza pia kwamba,watu wote ni sawa na hakuna kisingizio cha watu kutaka kunufaika na matukio yanayodharirisha umoja wa kitaifa . Na kwamba,  licha ya matatizo makubwa ya kiuchumi na uhaba wa rasilimali  na fedha, hizo si sababu za kufanya uharifu nchini  Misri.

Matamko kutoka kwa viongozi hawa wawili, Rais  al Sisi na Patriaki Tawadros, yalifuatiwa pia na kauli kama hiyo kutoka kwa Sheikh Ahmed al Tayyib, al Azhar Grande Imamu, ambaye pia aliutaka  umma wa Misri, kuheshimiana na kuung’oa mzizi wa fitina na vurugu kati ya makundi ya kidini.

Shirika la kujitegemea la Juhudi za Misri kwa Haki  Binafsi , limetaja  uwepo wa  matukio zaidi  77 ya ghasia za kidini katika mkoa wa  Minya tangu jaribio la 'mapinduzi ’ya  Januari 26, 2011. Na kwamba, kwa wakati huu, katika matukio mengi,  hatua za kisheria zimechukuliwa, kuwatambua na kuwafikisha mbele ya sheria  wote wanaohusika na ghasia,hasa kupitia juhudi za mikutano ya maridhiano, inayoandaliwa na utawala mahalia , kwa lengo la kuwaweka pamoja waamini na wanachama wa jumuiya mbalimbali za kidini, kwa ajili ya ujenzi wa amani. Na wengi wameipokea kama ni njia inayofaa kuchukuliwa kukomesha vurugu na ghasia.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.