2016-05-18 15:35:00

Papa aonya: kumpuuza mtu maskini ni kumdharau Mungu


 Mafundisho ya Baba Mtakatifu Francisko kwa mahujaji na wageni  kwa Jumatano hii, yametazama kwa kina hoja mbili :umaskini na huruma  ya Mungu. Ametoa tafakari kwa  maisha ya watu wawili, mtu tajiri na maskini Lazaro, walioishi maisha  tofauti kabisa  katika mizania ya maisha, na kusema kumpuuza mtu maskini ni kumdharau Mungu, na kwamba Huruma ya Bwana kwetu inakiungo thabiti na sisi kuwa na huruma kwa wengine.

Papa  alinukuu kama ilivyoandikwa katika Injili  ya Matayo , Maskini Lazaro daima alipenda kulala mbele ya  lango kuu la nyumba ya tajiri, akitamani  hata kula makombo ya chakula yaliyokuwa ya kidondoka kutoka meza  ya tajiri . Tajiri alivaa nguo anasa, wakati Lazaro alijifunika mwili wake uliokuwa umejaa vidonda kwa matambara yaliyochokaa. Tajiri kila siku alikula na kusaza wakati lazaro  akifa kwa njaa , wala hakuwa na mtu wa kuhudumia madonda yake badala yake mbwa walikuja kulamba madonda yake .

Baba Mtakaifu amesema, mfano huu  wa Lazaro na tajiri , unatukumbusha  maneno makali ya ujio wa pili wa  Yesu , ambamo alisema siku ya  mwisho wa hukumu , Mwana wa  Mtu atakapokuja tena kuwachukua walio wake na wasio wake atawaambia ”Mimi nilikuwa na njaa hamkunipa chakula, nilikuwa na kiu nanyi hamkunipa maji, nilikuwa [...] uchi hamkunivika " ( mt 25.42-43)”.

Papa anasema mfano wa maisha ya watu hawa wawili unatonyesha kwamba ,  Lazaro anawakilisha vizuri  kilio  cha kimya kimya cha baadhi ya maskini wa wakati wote na  hali tata za ulimwengu  ambamo  utajiri mkubwa wa rasilimali za dunia  umeshikwa na mikono ya wachache.

Papa ameendelea kueleza ilivyokuwa kwa watu  hawa wawili Lazaro na Tajiri walipokufa . Tunasoma kwamba kukawa na mageuzi makubwa ,  aliyekuwa maskini anakuwa tajiri na tajiri anakuwa maskini.  Lazaro anapa kutuzwa mbele ya uso wa Mungu na kuchuliwa na malaika na kulazwa katika kifua cha baba wa Imani Abraham .

Wakati mtu tajiri, alyeijiona amejitosheleza mwenyewe hapa duniani na kudharau  ya Mungu , sasa  anatupwa jehanamu katika mateso makali ya  njaa akitamani hata tone la maji lidondoke  ulimini  mwake, kutuliza kiu yake .  Lakini  Abraham anamweleza  kwa jinsi gani , utendaji wa haki na  huruma inavyokuwa kutimiza fumbo Takatifu la Mungu  linavyohusiana na  husiana na matendo ya huruma na kwa wengine .

Papa aliendelea kuonya kwamba,  kama ilivyokuwa kwa mtu huyo tajiri, milango ya mbingu imefungwa kwa wale ambao mioyo yao haiguswi na  mahitaji ya watu maskini.  Baada kifo na kutupwa jehananu mtu huyu tajiri ndipo anayafungua macho yake na kumwona Lazaro uwinginimikononi mwa Abrahamu.  Tajiri huyo anajaribu kuomba msaada lakini anaambiwa amachelewa . Hivyo kumbe Papa anasema wakati ni huu wa wa wogofu , wakati wa kufungua mioyo na kuuona ukweli wa neno la Mungu na ujumbe wake wa kuokoa ,  kama alivyoimba Mama Yetu Bikira Maria katika wimbo wake mkuu . Ni kufanya mabadiliko katika  maisha ya  dunia hii kwa ushindi wa haki na huruma ya Mungu.  Na  wogofu wetu tusiuegemeze katiak miujiza , bali tufungue mioyo yetu wai kwa neno la Mungu anayetutaka tumpende yeye na jirani zetu.

BabaMtaktifu alikamilisha Katekesi yake kwa maneno kwamba, Neno la Mungu lina nguvu ya kuuinua moyo uliopondeka na kuuponya upofu wake . Na kwamba Ujumbe wa Mungu wa una uwezo wa kuibadilisha sura ya dunia hii kwa ushindi wake wa haki na huruma. 








All the contents on this site are copyrighted ©.