2016-04-21 11:58:00

Papa asema Huruma ni ufunguo wa mlango wa kumfikia Mungu


Wajumbe wa Mkutano wa 38 wa Kitaifa wa Caritas Italiana, mapema Alhamis hii wamekutana na Baba Mtakatifu Francisko. Papa katika hotuba yake amekazia zaidi umuhimu wa kazi waliyokabidhiwa na kanisa tangu wakati wa kuanzishwa kwake mwaka 1972, katika kuhamaisha kanisa mahalia na wamini binafsi katika kuona maana na wajibu muhimu kutoa huduma na msada kwa watu wahitaji katika nyakati hizi zetu. Papa amewahimiza kama ilivyokuwa siku za nyuma hata leo hii,  katika uaminifu wa hisia mpya na uwajibikaji,  wanaendelea kutembea katika njia  mpya na ubunifu kwa ajili ya  kukabiliana na pia uhakiki unaolenga  kuimarisha na kutoa maelekezo yaliyo  bora zaidi katika yale yaliyokwisha fanyika tangu kuanzishwa kwake na jinsi ya kuyaendeleza.

Hivyo Papa ametaja kwamba utume wao umejikita katika  elimu, ambamo ni lengo la Caritas la siku zote katika ushirika wa  Kanisa na huduma katika mapana yake , lenye kudai  dhamira ya upendo thabiti kwa kilabinadamu, na hasa katika kutoa kipaumbele kwa  maskini ,kama Yesu alivyofundisha , kutoa msaada na kwa jirani na hasa  wahitaji zaidi (Mat 25.35-40). Upendo unaopaswa uonekane katika hatua zote za utendaji  wa Caritas na ishara zinazowakilisha mfano asilia wa kazi za ufundishaji za Caritas katika ngazi zote.  Papa alieleza na kuhimiza  ufundishaji kwa vitendo, na hasa katika lengo la kusaidia maskini kukua katika utu na  jamii ya Kikristo kutembea katika nyayo za Kristo pamoja na  vyama vya kiraia,  kwa uangalifu kukubali wajibu wao , kama Papa Benedikto XVI alivyosema katika hotuba yake kwa ajili ya maadhimisho ya kutimia miaka 40 ya  Caritas Italia, 24 Novemba 2011.

Aidha Hotuba ya Papa Francisko imegusia changamoto na utata wa wakati wetu, unaofanya kazi za Caritas kuwa ngumu  katika  kutoa msaada wake muhimu  kimatendo, na katika  kuhakikisha kuwa  ni huduma ya hisani inayodhamiriwa kwa  kila mtu, yaani, kwamba jumuiya zote za Kikristo kuwa walimu wa upendo, ili jamii nzima iweze kuchochewa kukua katika upendo wenye kutafuta  njia mpya za kuwa karibu na maskini wengi, uwezo wa kusoma na kukabiliana na hali ngumu na madhulumu yanayofanywa kwa  mamilioni ya watu  si nchini  Italia, Ulaya peke yake lakini  dunaini kote. Papa ameendelea kuwataka Wakristo kupitia chombo hiki cha Caritas, wawe kichocheo muhimu katika ujenzi wa uhusiano mzuri na taasisi za kiraia na uwepo wa sheria muafaka katika neema ya manufaa na utetezi wa makundi ya watu wanaoishi katika mazingira magumu zaidi.

Aidha Papa alitazama  dhamira ya upendo kwa jirani akiwaelekea  wakimbizi na wahamiaji. Tatizo la wahamiaji ambalo leo hii linawasilisha kipeo halisi kinachohitaji  uwepo wa sera  hai zenye kuona mbali zawadi ya utajiri  unaoandamana na wahamiaji na wakimbizi.  Kwa hiyo Papa amehimiza Caritas kuwa na ubunifu mpya kwa ajili ya ujenzi wa mshikamano  ulio thabti zaidi kati ya wakazi wa Italia na wageni ,  na uwepo wa mwendelezo  msingi wa utamaduni na ujuzi sahihi wa wataalamu , katika utatuzi wa mambo yanayoweza leta utata fulani  au kuwa na sura ya kipekee.

Papa alikamilisha hotuba yake kwa kuhimiza Caritas kutenda kwa ujasiri kamili mbele ya uso wa  Kristo Mfufuka na kwa ujasiri unaotoka kwa Roho Mtakatifu wenye kuwawezesha kusonga mbele bila woga na kugundua mitazamo mipya ya Maaskofu , na uimarishaji wa mfumo na motisha,inayoweza  kutoa jibu lenye  ufanisi zaidi kwa Bwana, anayeonekana katika nyuso za wahitaji,  wake kwa waume.  Papa alieleza na kuziweka kazi kwa Kanisa za Caritas  nchini ya maombezi ya Bikira Maria, na Mwenye Heri  Paulo  Paul VI.  Kwao wote aliwapa baraka zake za Kipapa na kuwaomba pia wamwombee.

Mkutano huu wa Caritas Italiana , umefanyika kwa  muda wa siku tatu mfululizo ,  18-21 Aprili 2016, katika jengo la Fraterna Domus la Sacrofano Roma, ikiwa ni Mkutano wa 38 wa  Kitaifa, ukiongozwa na Madakuu” Kuweni na Huruma kama Baba yenu alivyo na Huruma ( Lk 6, 36).   Mada hii iliyolenga moja kwa moja katika maadhmisho ya Jubilee ya mwaka Mtakatifu wa Huruma kama ilivyotangazwa na Papa Francisko kwamba: neno Huruma ni ufunguo wa mlango wa kumfikia Mungu kati yetu na katika kuwafikia wengine  hasa wanaoishi katika hali ngumu za kukata tamaa na waliosaulika pembezoni katika maisha ya kijami.

Mkutano huu umehudhuriwa na wajumbe kutoka matawi  yote 220 ya Caritas Italia ,pia kama sehemu ya kusherehekea miaka 45 tangu kuanzishwa kwake, na kama jukwaa la kupima utendaji wa kazi za kichungaji katika huduma ya watu maskini na kanisa nchini Italia, na katika mtazamo wa kutembea pamoja hata kwa siku za baadaye katika mwanga wa Waraka wa Kitume wa "Injili ya Furaha" na Mwaka wa Jubilee  ya Huruma na Waraka wa" Laudato Si". 








All the contents on this site are copyrighted ©.