2016-04-15 13:01:00

Maradhi ya akili ni moja ya sababu kubwa za uwepo wa walemavu wengi duniani


Watalaam wa maradhi ya akili, wameionya dunia kwamba,  magonjwa ya akili ni kati sababu zinazoongoza katika kusababisha uwepo wa ulemavu unaoathiri mamilioni ya watu duniani,ikiwemo migogoro ya kibindamu. Hivyo  huduma na tiba kwa wenye matatizo ya akili si suala la hiari au  kama anasa lakini ni muhimu kupewa kipaumbele. Wataalam walieleza wakati wa mkutano wa Benk ya Dunia na Shirika la Afya Duniani  uliofanyika wiki hii  Washington Marekani.  Mkutano pia ulifahamishwa kwamba idadi ya watu walioathirika na maafa yanayosababishwa na binadamu,  imeongezeka mara mbili katika kipindi cha muongo mmoja uliopita na idadi ya watu kuhama makazi yao  kuwa ni zaidi ya milioni 60 ikiwa ni juu zaidi tangu wakati wa  Vita Kuu ya Pili ya Dunia . 

Shirika la Afya la Dunia( WHO) linakadiria  maradhi ya akili, ikiwemo mfadhaiko, wasiwasi na hofu,  katika kipindi hiki kilichojaa migogoro ya kibinadamu, yanaonekana kuongezeka kwa asilimia  20 kutoka asilimia 10 katika nyakati tulivu za nyuma . Hivyo inaonyesha idadi ya watu walioathirika na maafa ya kibinadamu  imepanda duniani kote, na hivyo kuongeza mahitaji ya huduma katika afya ya akili. Ni maelezo yaliyotolewa na  Inka Weissbecker, wa Kitengo cha kimataifa  cha afya ya akili na mshauri wa kisaikolojia katika Shirika la Misaada la Kimataifa la Madaktari .

Watalaam wa afya walitoa maelezo wakilenga hali halisi za a afya ya akili za watu, kwenye nchi zilizokabiliwa na migogoro ya kivita kama vile Sierra Leone na Sudan Kusini . Na kwamba hadi hivi  karibuni, wafadhili kwa mfano nchini  Sudan Kusini, wanachukulia huduma ya afya ya akili  kama huduma isiyokuwa muhimu. Na wametaja unyanyapaaji  na ukosefu wa elimu kuwa  vikwazo vikubwa katika ufanikishaji wa huduma za afya ya akili  katika nchi zote, wengi hawajui kama magonjwa ya akili  yanaweza ponyeka  kwa matibabu, Dr Weissbecker alisema.

Na Mark van Ommeren, Mshauri  wa afya ya umma wa WHO,  juu ya masuala ya akili amesema: kuna takwimu za kutosha zinazoonyesha kwamba, kwamba,  afya ya akili ni tatizo kubwa katika  maisha ya wengi , kuliko hata ilivyokuwa siku za nyuma. Vita na majanga ya asili vimefungua mianya mingi inayoathiri akili ya mtu . Na hivyo ni muhimu kufungua  pia mianya mipya safi kwa ajili ya  huduma ya afya ya akili, kama kipengere muhimu pia katika kuboresha uchumi wa nchi na maendeleo ya jumla, alisema.

Nayo Matokeo ya Utafiti wa WHO yaliyochapishwa siku ya Jumanne, yanaonyesha kwamba kila dola moja inayowekezwa  katika kutibu mfadhaiko wa akili huzalisha dola 4 zaidi kutokana na ufanikisha wa afya bora na uwezo wa watu kufanyakazi .  Matibabu dhidi ya mfadhaiko wa akili unaotokana na hali za kuhuzunisha  na wasiwasi yana faida zaidi katika  maisha ya kijamii na kiuchumi pia kwa kuwa, huwezesha watu kufanya  kazi zaidi . Utafiti  huo umeonyesha mafanikio haya kwenye uhusiano wa karibu wa afya na faida ya kiuchumi kupitia uwekezaji  katika matibabu, kama ilivyoonekana kwenye nchi 36  zenye kipato cha chini, kati na juu zilizohusika kwenye utafiti huu,ikiwemo  Afghanistan na Sri Lanka ,  Burundi, mkoa wa Indonesia Aceh, Iraq, Jordan, Kosovo, Timor ya Mashariki, Lebanon na sasa Syria.








All the contents on this site are copyrighted ©.