2016-02-24 15:13:00

Katekesi ya Papa : Utajiri na madaraka vyapaswa kuhudumia watu wote.


Mafundisho ya Baba Mtakatifu Francisko , ya kila Jumatano kwa mahujaji na wageni, yameendelea kuizungumzia huruma  ya Mungu  katika huduma kama ilivyoandikwa katika  Maandiko  Matakatifu. Papa amerejea  Agano la kale akianisha na Agano jipya vifungu  vinazungumzia   nguvu za  Utajiri, Ufalme,  na  wenye mamlaka ya juu , na pia ya kiburi cha majivuno na ukatili wao.

Baba Mtakatifu amekiri ukweli  kwamba,  utajiri na mamlaka vina nguvu ya kutengeneza  mazuri  lakini tu kama vitatumiwa kwa  manufaa ya wote, hasa iwapo vitatumika kama huduma kwa haki na upendo kwa watu wahitaji,  hasa  maskini.  Bahati mbaya aliendelea , uzoefu  mara nyingi umeonyesha utendaji tofauti na huo, utajiri ukitumika  kama nafasi ya kutoa  upendeleo  kwa wenye navyo matajiri , na kujenga hali ya kugandamiza wasiokuwa navyo, ubinafsi na nguvu na hata kusababisha uwepo wa rushwa na  hata mauaji,  kama ilivyotokea katika shamba la mizabibu la Nabothi, ilivyoelezwa katika kitabu Kwanza cha Wafalme Sura ya 21, ambamo Naboth ,anatendewa kinyume  cha haki, kunyang’anywa  shamba lake na kuuawa  ili Mfalme Ahab , amiliki aridhi yake.

 Papa alitazama kwa kina maelezo hayo na kusema kuwa  Yesu leo hii anatutaka  kuwa tofauti na roho hiyo, anatutaka kuonyesha ukuu si kwa kugandamiza, lakini kwa unyenyekevu wa kujaliana mmoja kwa mwingine.  Alieleza kwa kurejea  maneno ya Yesu, kwa wanafunzi wake alipowaonya  wasitawale kwa kugandamiza lakini uwezo wa mamlaka na uongozi iwe ni huduma ” yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu ni lazima awe mtumishi wenu, na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu lazima awe mtumwa wenu “(Mt 20.25-27). Papa amesema kwa mtawala anayepoteza  mwelekeo wa huduma, basi  nguvu yake humezwa na kiburi cha  unyanyasaji kama kile kilichotokea katika shamba la mizabibu la Nabothi. Yezebeli, kwa njia za hila anaamua kumwondoa Nabothi  ili atekeleze mpango wake dhalimu, wa mfalme  kumiliki mali ya Nabothi.  Huu ni ukaidi na majivuno ya mamlaka yasiyo heshimu maisha , ni utawala usiokuwa  na haki wala huruma. Ni  kiu ya kutawala wenye kujenga moyo wa  uchoyo na ubinafsi wa kutaka  kumiliki kila kitu. Lakini  Bwana anaonya juu ya tamaa  hizo za wenye mamlaka na  matajiri, akisema , ole wenu ninyi mnaotaka kujiongezea utajiri wa   nyumba  hadi nyumba, kuongeza shamba hadi  shamba, mpaka hakuna nafasi zaidi ya kukaa wengine na hivyo mnabaki peke yenu (Isa 5,8).

 Na kwamba , Yesu anatuambia kwamba ni lazima kuonyesha ukuu wwetu si kwa klugandamiza wengine lakini kwa kutumikiana kwa unyenyekevu, mmojakw amwingine. Na kwama Bwana alivyomtuma Nabii Elia kumtaka Ahab atubu dhambi zake , pia alimtumwa mwana wake pekee kutuonyesha huruma yake ya kuokoa  yenye kutuweka huru dhidi ya dhambi na ukosefu wa haki . Huruma huwa na uwezo wa kuponya dhambi n aina unaweza kubadilisha historia ya maisha yetu. Hurma ya Mungu ni nguvu kuliko dhambi ya binadamu.  Nguvu ya Yesu yakuokoa huonekana katika mti wa Msalaba wa Yesu.  

Papa alikamilisha na ombi kwamba, katika mwaka huu Mtakatifu, na tumwombe Bwana ajongee  karibu zaidi wadhambi , na kutuonyesha huruma yake  yenye  kutukomboa katika hali nyingi za ukosefu wa haki katika dunia hii yetu,  kwa uwezo wake huruma yake na msamaha.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.