2016-02-15 14:10:00

Mamia ya watu wamzika Marehemu Mstaafu Askofu Kakubi wa Mbarara


Mamia ya Wakatoliki na wasio Katoliki wa Jimbo Kuu la Mbarara, mwishoni mwa wiki walisongamana katika Kanisa Kuu la Nyamitanga wakiongozwa na Askofu Mkuu Paulo Bakyenga , kutoa heshima zao za mwisho na mazishi ya Askofu Mstaafu  John Baptist Kakubi wa Jimbo Kuu la Mbarara. Askofu Mstaafu Kakubi alifariki dunia Alhamis ilyopita katika Hospitali ya Kimataifa ya mjini Kampala, akiwa na umri wa miaka 87.

Ibada ya Misa ya Wafu , iliongozwa na Askofu Mkuu Paul Bakyenga katika Kanisa Kuu la Nyamitanga na baadaye ibada ya mazishi  katika  Kanisa dogo la Kituo cha Malezi ya Kiroho cha Mtakatifu Yosefu  kwa matashi yake Marehemu.  Kituo alichokianzisha ambacho alikuwa akivunia uwepo wake wa miaka 35 kuweza kutoa matunda ya watalaam wengi wa ngazi za juu , wakiwemo mapadre, madaktari  na wanasheria.

Maaskofu wengine waliohudhuria maziko haya ni pamoja na Askofu  Vincent Kirabo wa Jimbo la Hoima Askofu John Baptist Kaggwa wa Jimbo  la Masaka, Askofu  Callist Rubaramira wa Jimbola Kabale Askofu , Robert Muhirwa wa Jimbol a fort Portal Askofu Egidio Nkaijanabo wa Jimbo la Kasese,  Askofu  Lambert Bainomugisha  Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Mbarara naAskofu Mstaafu  Edward Baharagate wa Jimbo la Hoima.  Pia walihudhuria viongozi wa makanisa  na mani zingine akiwemo   kutoka Dayosisi ya Kianglikani ya Ankole Askofu Sheldon Mwesigwa,  pia Kadhi wa Wilaya wa Mbarara, Sheikh Ramadhan Khamis na mtangulizi wake Sheikh Abdu Noor Kaduyu. .

 Askofu Bakyenga , katika homilia yake alimtaja Marehemu Askofu Kakubi kuwa  mfano wa kuigwa na viongozi wa kanisa, waamini na watu wote katika kuwa mtu mpole na  adilifu. Kwamba alikuwa ni mtu mwenye bidii katika maombi, na mwenye kujituma.

Habari zake binafsi zinasema, alizaliwa  Septemba 23, 1929, kijijini Kyanda, Rugaaga, Parokia ya Birunduma ambayo sasa ni Wilaya  ya Isingiro.  Alisoma  Shule ya Msingi ya Birunduma na  Nyamitanga na semnari ndogo ya  Kitabi Bushenyi, na baadaye Seminari  kuu ya  Katigondo Masaka, na St Edmund ya Allen Hall, Uingereza.

Baada ya kupadirishwa alifanya utume wake katika Paroliki  ya  Nyamitanga, kisha Seminari ya Kuu ya Katigondo na  Kitabi . Aliteuliwa kuwa Askofu wa Jimbo la Mbarara Julai 5 1969 na  Septemba 7, 1969 alsimikwa kuwa Askofu wa Mbarara.  Mwaka 1980, alianzisha Shule za Malezi  za  Mtakatifu Yosefu na Cha Mtakatifu Cecilia

Alistaafu  kazi za kichungaji za jimbo mwaka 1991, bada ya kutumikia kama  Padre kwa miaka  55 na 47 kama Askofu.  Mungu ailaze Roho yake pema Peponi. 








All the contents on this site are copyrighted ©.