Jumapili, Baba Mtakatifu Francisko akihutubia maelfu ya mahujaji na wageni waliofika katika Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro , kwa nia ya kusali pamoja nae sala ya Malaika wa Bwana, kabla ya sala hiyo, alitoa tafakari fupi juu ya somo la Injili, ambalo linazungumzia wito wa Yesu kwa wafuasi wake wa kwanza, akiwa kando ya Ziwa Galilaya. Wafuasi hao wa kwanza ambao walikuwa wavuvi , wakiwa katika hali ya kukata tamaa baada ya kuvua usiku mzima bila kupata samaki, walianza kuweka nyavu zao sawa, ili warejee makwao . Yesu anaingia katika mashua ya Simon Petro na kuhubiri umati wa watu waliokusanyika katika pwani ya Ziwa Galilaya .
Baada ya kuhutubia Yesu anamwambia Petro, kutweka nyavu kilindini, ili wapate samaki. Na Petro anamjibu Yesu , kwamba wamefanya hivyo usiku wote na hawakupata kitu , lakini akaonyesha imani yake kwa Yesu na kusema , kwa maneno yako, tunaweka tena nyavu kilindini.Papa anasema imani ya Petro kwa maneno ya Yesu iliwapa zawadi ya samaki wengi , waliotaka hata kukata nyavu!
Wakiwa katika hali ya kushangalia maajabu hayo, Petro alijiona mnyonge na kuanguka miguuni pa Yesu akisema, "Ondoka mbele yangu Bwana, kwa kuwa mimi ni mwenye dhambi. Petro, alieleza Papa, anapata kufahamu kwamba Yesu ni Bwana na anapata hisia kali kwamba , hawasikustahili kuwa mbele za Bwana. Lakini Yesu anamwambia: "Usiogope, tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu". Papa alisema Yesu hakuondokana kumwacha Petro katika dhambi zake , bali alimtakasa na kumfanya kuwa mfuasi wake, upendo wa Yesu unakuwa zaidi ya daktari anayemhudumia mgonjwa na kumwacha.
Papa alisema , maneno ya Yesu kwa Petro na wanafunzi wengine , ni kiini cha huduma ya Yesu na utume wa Kanisa. Na alifafaanua kwamba, kwenda kuvua watu, wake kwa waume haina maana ya kuwalazimisha wengine kumwongokea Yesu, lakini ni kurejesha heshima na uhuru wao kupitia msamaha wa dhambi. Hicho ndicho kiini cha Ukristo. Ni kushiriki upendo unaotolewa bure na kuendelea kukua ndani na Mungu kwa njia ya ukarimu na huruma kwa watu wote.
Baada ya hotuba hiyo , Papa alisali sala ya Malaika wa Bwana. Na alikamilisha tukio hili kuizungumzia kidogo pia ziara yake ya kitume nchini Mexico na Cuba , anayotazamia kuianza mwishoni mwa wiki hii, ambamo pia anatazama kukutana na Patriaki Kirill, Mkuu wa Kanisa Kiotodosi la Moscow na Urusi yote. Papa pia aliwakumbusha waamini katika Jumatatu katiak sala zao kuwakumbuka wahanga wote wa utumwa mambo leo. Mama Kanisa , ameadhimisha Siku kuu ya Mtakatifu Bakhita, kwa kuwaombea wote wanaoishi katika hali za udhalimu wa utumwa mambo leo kinyume. Pia aliomba wakati huu wa mapambazuko ya mwaka mpya , amani na utulivu vitawale kwa wote na kwa namna ya kipekee alilitaja Taifa la China ambalo Jumatatu hii, limeadhimishwa Siku Kuu ya Mwaka Mpya , kwa mujibu Kalenda ya China.
Aidha Papa , kwa mara ingine alitoa ombi kwa Jumuiya ya kimataifa, ione haja ya kutenda kidharura, kurejesha amani nchini Syria. Aliomba kila juhudi ifinyike kufanikisha mazungumzo ya pamoja kwa pande zote zinazo husika katika mzozo huu wa Syria, waketi pamoja katika meza ya mazungumzo na kutoa jibu moja muafaka kwa wote, linaloweza sitisha ukatili unaofanyika hasa kwa raia wanyonge wasiokuwa na usemi nchini Syria . Kwa ajili hiyo, Papa aliomba sala za wote , ziwakumbuke raia hawa wa Syria waliojikuta wamezingira na mapiganoya kivita, yanayo kuacha kila kitu kwa hofu wakikimbia dhuluma za vita na kupoteza maisha yao.
Papa aliomba “mshikamano na ukarimu”, hasa katika upatikanaji wa mahitaji ya lazima kwa wakimbizi hawa, na kuhakikisha wanaishi katika hali ya maisha yenye heshima.. Na wakati huohuo jumuiya ya kimataifa ifanye kazi kwa haraka zaidi, kupata ufumbuzi wa vita hivyo , kupitia njia ya mazungumzo . Alisisitiza ni tu majadiliano katika meza moja yanayoweza kupata ufumbuzi katika kinzani za kisiasa na kuhakikisha uwepo wa maridhiano na amani kwa taifa hilo la Syria.
Papa Francisko alikamilisha ombi lake kwa Jumuiya ya kimtaifa akiomba pia watu wote kusali kwa ajili ya amani nchini Syria,na kuwa tayari kuwapokea wakimbizi wanaotafuta hifadhi na aliomba maombezi ya Bikira Bikira Maria, Malkia wa amani.
All the contents on this site are copyrighted ©. |