2016-02-01 13:59:00

Afrika yatakiwa kutekeleza maazimio ya kukabiliana na mbadiliko ya tabia nchi


Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika,  Dk Nkosazana Dlamini-Zuma ,  akizungumza katika  Kikao cha kawaida cha 26 cha Baraza la Wakuu wa Nchi na Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia, Jumamosi na Jumapili iliyopita,  alitoa  wito kwa nchi zote za Afrika, kuona  dharura ya kuwa na mipango ya haraka, kutekeleza  yaliyokubalika katika  prokali ya Kimataifa ya kukabiliana na mabadiliko hasi ya tabia nchi .

Licha ya kutambua  kwamba,  Afrika haichangii  kwa kiwango kikubwa  kimataifa , uharibu  wa mazingira , bahati mbaya, ndilo bara linalo athirika vibaya  zaidi na mabadiliko hayo . Hivyo ni lazima kupania kutekeleza hatua zote zinazoweza boresha hali ya hewa , ikiwemo  kilimo safi na  nishati mbadala, ili kuokoa maziwa, misitu, bahari na mito ya Afrika , na  kupambana kwa uhakika zaidi dhidi ya majanga ya asili na hatari zingine za mabadiliko ya tabia nchi.

Mwenyekiti  Dlamini, aliomba uwepo wa kasi  katika dhamira mpya za utendaji barani  Afrika,  kuonyesha ukomavu  baada ya  kupita kipindi cha miaka 50, tangu kuundwa kwa  AU, kwa lengo la kuwa na umoja katika kuleta mafanikio na amani na ustawi wa watu barani Afrika, wakisukumwa na kuongozwa na nguvu ya za wananchi. Na pia  kama walivyokubalina katika ajenda  za hadi mwaka  2063, katika  kuleta  mabadiliko mapya Afrika.

Alieleza na kuwasisitiza viongozi wenzake kwamba , ni kuanza sasa  kuongeza kasi ya mageuzi  kwa katika mwaka huu  2016, ambao ameutaja kuwa  jukwaa la kuendeleza haki za binadamu kwa  wakazi wote wa bara la Afrika katika utofauti wao wote.  Na kwamba katika  mwaka huu 2016, ambao umetajwa maalum kwa ajili ya utetezi wa Haki za Binadamu, ukilenga hasa kukuza  haki za wanawake na wasichana, ni lazima kuongeza kasi ya mabadiliko. Ni lazima kuendelee kuweka watu wote  na haki zao za msingi ,kama kituo  kikuu rejea katika ajenda kufikia  2063.

 Alikumbusha ,  ni pamoja na haki za watu  kupata elimu, chakula na lishe, huduma za afya, huduma  salama maji, usafi wa mazingira na nishati, maisha tulivu na  amani,  dhidi ya ukatili na msimamo mikali, haki ya uhuru wa kujieleza, uhuru wa vyombo vya habari na ulinzi dhidi ya ubaguzi wowote ule.

Pia alimewataka viongozi wa Afrika , kuhakikisha wanapima mambo kwa hekima kubwa  kabla ya kutoa maamuzi yao katika hoja na  matakwa ya watu wa Afrika, na katika kutatua matatizo ya Afrika , kwa manufaa ya sasa na kwa vizazi vijavyo.

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.