2016-01-12 12:06:00

Kwa imani thabiti sala na maombi hutenda miujiza


Mabadiliko katika Kanisa hayaletwi na sala za Mapapa au Maaskofu au Mapadri peke yao lakini huletwi na sala na maombi ya waamini Wakatifu wa Kanisa. Na kwa sala na maombi miujiza hutendeka na huwa na uwezo kuilainisha mioyo migumu, hata  iliyosahau huruma ya Mungu. Ni msisitizo wa Mahubiri ya Baba MtakatifuFrancisko, mapema  Jumanne hii wakati wa Ibada ya Misa aliyoiongoza katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta mjini Vatican. .

Homilia ya Papa ililenga kutoa ufafanuzi juu ya masomo ya siku hasa kutoka  Kitabu cha Samueli  linalozungumzia Mwanamke Anna, mwanamke  tasa ambaye  hakuchoka kutoa maombi  na kilio chake kwa Mungu,akiomba kujaliwa mtoto. 

Papa ameutaja ujasiri wa sala katika imani kama ilivyokuwa kwa  Anna, licha ya hali yake mbaya ya kimaisha kwamba, sala zake zilitoka ndani ya moyo wake,  midomo yake ikionekana  kunena lakini bila sauti yake kusikika, hata kuonekana kama vile ni mlevi wa mvinyo .  Papa anasema  ameutaja ujasiri huu wa Anna katika kuomba  neema ya Bwana, kuw ani ujasiri katika imani. Kwa hisia hizo Papa Francisko,amewakumbuka wanawake wengi  wema ndani ya Kanisa  ambao hutoa maombi ya kwa Mungu kwa jasiri na bila kuchoka ,ingawa mara nyingi  Kanisa haliwatambui wala kufanya rejea kwao. Amesema ni wanawake wachache tu  wanaokumbukwa na Kanisa katika ujasiri wa maombi na sala kama Mtakatifu Monica ,ambaye kwa machozi yake aliweza kupata neema ya kuyaongoa maisha ya mwanae Mtakatifu Augustine. Lakini kumbe kuna wanawake wengi wa namna hiyo.

Aidha Mafundisho ya Papa yalimwelekea  Kuhani Eli, mtu maskini  ambaye Papa  Francisko, anamwonea huruma na kusema anamkubusha mapungufu yake, na kumpa ufahamu zaidi , wa kutambua jinsi gani ilivyokuwa vyepesi kuhukumu watu wengine kwa jinsi wanavyoonekana  bila  hata ya kujiuliza kwa kina wanayo fikiri nini  mioyoni mwao?  Na kwamba pale  panakosekana huruma ndani ya moyo, daima fikra huelekea katika uovu ,wenye kumweka mtu mbali na mbali na yule anayesali kwa  maumivu na  uchungu ,ambaye  huweka dhamana maumivu na uchungu huo kwa Bwana.

Baba Mtakatifu Francisko aliendelea kulinganisha maumivu na uchungu katika sala  kama ilivyokuwa kwa Yesu katika bustani ya Mizeituni, aliposali kwa uchungu  na maumivu  makubwa,  lakini kwa radhi na unyenyekevu alisema, Baba, si kwa mapenzi yangu lakini utakalo lifanyike.  Hivyo tunaona kwamba, Yesu pia alitembea  katika maumivu na uchungu wa sala kama  ilivyokuwa kwa  Anna, kuomba kwa unyenyekevu mwingi bila kukoma. Na  hivyo ndivyo inavyotakiwa ,kutolea sala zetu kwa upole na unyenyekevu na kumwachia Mungu, mwenywe atoe jibu lake kwa jinsi anavyoona inatufaa.   Papa anasema  hakuna kukata tamaa ,ni kuendelea kuomba neema ya Mungu kwa  uchungu wote wa moyo  hadi kupata jibu .

Papa alieleza na kutoa mfano mwingine wa baba mmoja huko Buenos Aires, ambaye binti yake mwenye umri wa 9 alikuwa katika  hatua za mwiso wa maisha yake hosptalini alikokuwa amelazwa , ambaye usiku mzima, baba huyo alikesha katika lango la Madabahu ya Mama Bikia Maria wa Luján akiomba neema ya binti yake kupona ambaye  siku iliyofuatia,alimkuta mwanae hospitalini akiwa ameponywa kimiujiza. Papa alieleza na kukamilisha homilia yake na himizo kwamba ,watakatifu ni wale ambao wanaamini kwamba, Mungu ni Bwana na anaweza fanya jambo lolote. 

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.