Kuweni visima vya huruma ya Mungu na hasa katika kujali mahitaji ya wahamiaji, ambao wengi wao wanahitaji kukaribishwa . Ni ujumbe wa Baba Matakatifu Francisko, uliotumwa kwa vijana wa Jumuiya ya Taize, zaidi ya 30 elfu walikusanyika Valencia, Hispania, kwa ajili ya Mkutano wa 38 wa Vijana wa Taize Barani Ulaya. Mkutano huu wa vijana wa Taizé, ambao hufanyika katika mazingira ya kiekumene, umeanza Jumatatu hii Desemba 28 na utakamilika tarehe Mosi, Januari 2016.
Ujumbe wa huo uliotiwa saini na Katibu mkuu wa Vatican Kardinali Pietro Parolin, Papa amewashukuru vijana wa Taize, kwa uchaguzi wao wa kujiunga katika mkutano wao wa mwaka huu, unaoongoza na mandhari ya Huruma na Shukurani , katika utendaji wao wa kazi zao, na katika mtazamo wa juhudi na nguvu zote za ubunifu na mawazo yao kama vijana. Papa anashukuru moyo huo wenye kuonyesha nia ya kutambua umuhimu wa huruma kuwa kigezo cha kuonekana wazi wazi katika vipimo vyote vya utendaji wao pamoja na utendaji wa jamii kwa ujumla.
Ujumbe wa Papa unaendelea kuwatia moyo vijana waendelee kutembea katika njia hiyo ya kuwa jasiri wa kuhudumia kwa huruma, akisema si tu huwawezesha kupokea baraka wao wenyewe tu na maisha yao binafsi , lakini pia kwa jirani zao na wale walio katika hali ngumu. Aidha alimewakumbusha , Kanisa lipo kwa ajili ya binadamu wote , na ni mahali ambapo huruma ya Mkristo, ni kwa kila binadamu, na hivyo Kanisa linakuwa ni kisima cha huruma kwa kila mtu. Na ndivyo jumuiya yao ya Taize inavyopaswa kuwa. .
Mwisho wa Ujumbe wake, Papa Francisko, alimkumbuka mwanzilishi wa Jumuiya ya Taize , Bruda Roger, hasa jinsi alivyowapenda watu masikini , na wasiojiweza, wale walioonekana hawana maana kwa wengine, yeye aliweza kuonyesha kupitia maisha yake kwamba njia ya sala huenda sambamba na mshikamano wa binadamu. Na hivyo Papa amewataka vijana pia kupitia uzoefu wao katika mshikamano na huruma , waweze kuishi maisha hayo kwa furaha kuu , katika maana ya utajiri wake wa kiroho, kama ulivyo wito wa kila mmoja wao katika kuitumikia Injili.
All the contents on this site are copyrighted ©. |