2015-11-27 14:57:00

Hakuna shida kwa Wakristo na Waislamu kuishi pamoja kwa amani


Umoja , mshikamano na amani kati ya Wakristo na Waislamu barani Afrika , siyo tu vinawezekana, lakini ni ukweli halisi, kwa kuwa hakuna dini yenye  kuwa na uwezo wa kufuta dini nyingine. Ni maelezo yaliyotolewa hivi karibuni na Askofu Mkuu Ignasius  Kaigama wa Jimbo Kuu la Jos  Nigeria, ambaye pia ni Rais a Baraza la Maaskofu Katoliki Nigeria. Askofu Mkuu Ignasius Kaigama alieleza hilo, katika mhadhara wa Chuo Kikuu cha DePaulo cha Marekani hivi karibuni juu ya Mada "Waislamu na Wakatoliki katika  Mazungumzo: Matarajio, Fursa na Changamoto. Mhadhara huo uliandaliwa na Kituo Katoliki cha Utamaduni  na Theolojia katika Chuo Kikuu cha DePaulo.

Katika Maelezo yake aliisisitiza kwamba, "Ukristo na Uislamu  lazima kutembea  pamoja kwa kuwa waamini wa dini hizi mbili wote hutumia "Neno amani.  Amani  kama moja ya nguzo muhimu  katika imani ya  dini hizi.  Daima  huhimiza amani na  kamwe vita.  Kwa imani hiyo, mazungumzo kati ya makundi haya mawili , yanawezekana na hakuna  sababu  zinazoweza tosheleza kusema  yasiwepo,  iwapo wote wanazungumza lugha moja ya amani.  

Maelezo ya Askofu Mkuu Kaigama, yalionyesha pamoja na uwepo wa migogoro mingi na vurugu, katika ukweli wake wa ndani hakuna sababu za kidini lakini ni vurugu  na migongano inayolishwa na chuki za kisiasa au kikabila na  masuala mengine yanayosababisha umaskini na uhaba wa rasilimali, ingawa inaweza pambwa na watu kama ni migongano ya kidini.

Askofu Mkuu Kaigama,  alionya kila mmoja kushikilia imani yake,  kama njia iliyo bora katika kuyaongoza maisha bila kuingilia imani ya wengine.  Na alihitimisha kwa kutoa ombi kwa viongozi Wakristo na Waislamu 'kuhakikisha hakuna uhasama wala vurugu katika kukabiliana tofauti zinazoweza jitokeza,  badala yake watumie njia ya majadiliano na kuheshimiana .

Na Ijumaa  hii Novemba 27, majira ya jioni katika  Chuo Kikuu Katoliki ya Moyo Mtakatifu  cha Milan, katika ukumbi wa  Pius XI,  kutafanyika Mkutano kuzungumzia  : Mipaka katika mabadiliko:  Ulaya na Uislamu baada ya mashambulio ya kigaidi ya Paris.  Kati ya watakaotoa mchango katika mkutano huu ni Askofu Mkuu wa Milan, Kardinali Angelo Scola. Wengine watakaotoa mchango ni Profesa Abdelmajid Charfi, Mkuu wa zamani wa Kitivo cha Sayansi ya Binadamu, katika  Chuo Kikuu La Manouba, Tunis, pia  Profesa Henry Laurens wa Chuo de France cha Paris, na Profesa Riccardo Redaelli wa Chuo Kikuu  Katoliki cha Moyo Mtakatifu cha Milan.

Mjadala utazinduliwa na  Profesa Franco Anelli, gombera wa Chuo Kikuu Katoliki, na mwanasheria Giuseppe Guzzetti, mwenyekiti wa  Shirika la Cariplo. Mjadala wa mahusiano kati ya Ulaya na ulimwengu wa Kiislamu, unalenga hasa kutafakari na kutoa jibu la pamoja kwa  haraka zaidi,  baada ya mashambulizi ya kutisha huko Paris. 








All the contents on this site are copyrighted ©.