2015-11-16 09:24:00

Tafuteni kuongozwa na Yesu na si kuongozwa na wapiga ramuli na waaguzi


Jumapili wakati wa Sala ya Malaika wa Bwana, katika hotuba yake fupi kwa mahujaji na wageni waliofika kumsikiliza katika Uwanja wa Kanisa Kuu la Matakatifu Petro, , alielekeza hotuba zaidi katika masomo ya  Jumapili, yaliyoashiria kukaribia kwa  mwisho wa mwaka wa Liturujia ya Kanisa. Masomo ,  yaliyogusia ufunuo katika  ujio wa ufalme wa Mungu katika 'nyakati za mwisho'.

Tafakari ya Baba Mtakatifu Francisko alilenga zaidi katika lengo la mwisho la maisha yetu hapa duniani, kwamba ni kukutana na Kristo Mfufuka. Papa alieleza huku akihoji ni  wangapi ambao hufikiri juu ya hili?  Na akasema tatizo si lini dalili za maonyo ya kinabii juu ya mwisho wa dunia lini zitaanza kuonekana, lakini  hasa ni iwapo kweli tupo tayari kuukabili mwisho wa dunia.  Na vivyo hivyo , tatizo si jinsi mwisho wa dunia utakavyotokea lakini hasa jinsi tunavyopaswa  kuuishi wakati huo.

Papa alieleza na kutoa wito kwamba, tangu sasa tunatakiwa kuyaishi matukio hayo  kama inavyopaswa kwamba ni kuyajenga maisha ya baadaye kwa utulivu,  uaminifu na kumtumaini  Mungu. Hata hivyo akaongeza, ingawa ni vigumu kuishi kwa  matumaini , lakini inawezekana kwa kutazama kwa  nguvu  sura ya  Kristo Mfufuka, kwa kuwa Yesu si tu hatima ya njia yetu ya hapa duniani , lakini ni Yeye Yesu mwenye we huongozana na  sisi katika maisha yetu ya  sasa kila siku,  akitafuta kutuokoa na  manabii wa uongo na mawazo maovu.   Papa alieleza na kuwauliza waliokuwa wakimsikiliza ni wangapi wanategemea kuongoza na wapigabao au wapiga ramli, badala ya kuomba kuongozwa na Yesu, ambaye daima yumo katika kuliishi Neno lake lenye kuongoza na ambaye daima hubaki na sisi.

Baada ya hotuba yake, Papa aliwakumbuka wahanga wa shambulio la kigaidi lililotokea Paris Ufaransa siku ya Jumamosi, shambulio alilolitaja kuwa ni  unyama wa hali ya juu.

Na baadaye , kwa njia ya telegramu , alipeleka salaam zake za rambirambi kwa  Kardinali André Vingt-Trois, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Paris, akimhakikishia ukaribu wake kwa waathirika, familia zao na wafanyakazi wa dharura kwamba yuko pamoja nao katika  maombi. Salaam hizi za Papa zilizotiwa saini na Kardinali Pietro Parolin Katibu mkuu wa Vatican.  Papa Francisko amelaani vikali vitendo vyote vya vurugu, na kumwomba Mungu neema ya  kuhamasisha mawazo ya amani na mshikamano. Na amemwomba Mungu, Baba wa huruma, awapokee   waathirika katika amani ya Nuru yake na kuwapa faraja na matumaini  majeruhi wote na  familia zao.  Pia aliwataja wote walioshiriki katika kutoa msaada kwamba kwao wote yu karibu nao kiroho. Kwa mara nyingine tena,  Papa alirudia kusema kwa nguvu kulaani vurugu, akisema , haiwezi kutatua jambo lolote. 








All the contents on this site are copyrighted ©.