2015-11-16 08:29:00

Papa: Wakatoliki, Walutheri ni lazima kusahau ya nyuma na kufanya kazi pamoja


Wakatoliki na Walutheri wametakiwa  kuomba msamaha na kusameheana  kati yao kwa  ajili ya  kashfa ya mgawanyiko wa siku za nyuma, hasa kwa wakati huu wanapo tembea pamoja katika utumishi wa maskini na wahitaji. Ilikuwa ni  kiini cha ujumbe wa Papa  alioutoa siku ya Jumapili iliyopita, wakati alipotembelewa  na  Viongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la  Roma, kwa ajili ya kuwa na Ibada ya sala ya jioni kwa pamoja. .

Baada ya kujibu maswali  kadhaa yaliyoulizwa na wageni wake , kutoka  jumuiya ya Kilutheri ya Roma , Papa Francisco alizungumzia jinsi Yesu kiongozi wao  wote,  anavyowaongoza katika njia ya kutembea pamoja kwa upendo kupitia huduma mbalimbali kwa maskini katika moyo wa maisha ya Kanisa na huduma.

Hotuba ya Papa alikumbuka adha na madhulumu ya siku za nyuma yaliyofanywa na Wakatoliki na Walutheri,  dhidi ya kila mmoja ,  akisema kwamba leo ni lazima kuomba msamaha na kuchagua kutumikia pamoja, kama vile Yesu alivyoamuru kutumikiana mmoja kwa mwingine kwa upendo na umoja kamili” Baba naomba hawa ulionipa wawe na umoja kama sisi tulivyo na umoja” .  Papa alieleza na kumwomba Bwana , asaidie makanisa haya kutembea pamoja, badala ya kulenga katika  mgawanyiko . Aliomba uwepo wa upatanifu katika tofauti zinazo watenganisha  katika utumishi na hasa kwa wale wanaohitaji zaidi.

Aidha Papa alizungumzia umhimu wa kuwa na  ibada za pamoja  na matukio mengine ya Wakristo kuabudu pamoja. Alieleza hili huku akiirejea  Wiki ya Sala kwa ajili ya Kuombea Umoja wa Wakristo, tukio la kila mwaka mwezi  Januari na Siku ya Sala kwa ajili ya Viumbe ya Septemba 1 , kwamba ni matukio mawili ambamo Wakatoliki na Walutheri unaweza kusonga mbele zaidi katika njia hii ya moyo wa kiekumeni.

Mwisho wa maelezo yake Papa alisema “ ni muhimu kwamba Kanisa Katoliki linaendelea kwa ujasiri na kwa uaminifu,  kutathmini upya nia za  kuwa na Mabadiliko ndani ya  Kanisa na kwa namna ya kipekee katika  wazo la Martin Luther , aliyedai kwamba Kanisa daima ni lazima  kuwa na marekebisho.  Alieleza kwa kurejea hati ya pamoja inayoandaliwa kwa wakati huu  kwa ajili ya Maadhimisho ya Walutheri ya  Mabadiliko katika Kanisa  'Kutoka  migogoro  hadi Ushirika :Walutheri na Wakatoliki katika Maadhimisho ya  Mabadiliko  ya Kanisa  2017'. Papa amefurahia juhudi hizo akisema ni njia nzuri yenye matumaini.

Hii ilikuwa ni mara ya tatu kwa Papa Francisco kutembelea na viongozi wa Kanisa la  Kiinjili la Kilutheri Roma, kama pia ilivyofanyika kwa watangulizi wake, Mstaafu Papa  Benedict XVI, Machi 2010 na Papa  Yohana Paulo II,  Desemba 1983, kuashiria miaka mia 5 ya kuzaliwa Martin Luther.








All the contents on this site are copyrighted ©.