2015-10-22 15:07:00

Mazungumzo kina kwa kuheshimiana na kusikilizana ni ufunguo wa mafao ya wengi


Baba Mtakatifu Francisko, kwa njia ya telegramu iliyotiwa saini na Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican, amepeleka salaam na ujumbe wake kwa Askofu Nazzareno Marconi, wa Jimbo la  Macerata - Tolentino - Recanati - Cingoli - Treia, juu ya tukio la mkutano wa kimataifa  wa Matazamio mapya kutoka tafakari Padre Matteo Ricci.  Mkutano huu wa Kimataifa wa siku tatu Oktoba  21 hadi 23, umeandaliwa na  Chuo Kikuu Macerata na Taasisi ya Confucius Macerata.

 Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake ameonyesha furaha yake na  kutoa shukrani kwa hatua  hii ya kuimarisha  kazi ya kimisionari na utamaduni watu Macerata, wapenzi wa rafiki wa watu wa China. Na kwamba utakatifu wake  Padre Ricci ,umetengeneza mfumo wa uhusiano kati ya utamaduni wa Ulaya na China, wenye kuthibitisha umuhimu wa mazungumzo kati ya tamaduni na dini katika kuheshimiana kwamba huzaa matunda kwa  manufaa ya wote. Kwa hisia hizo, Ujumbe wa Papa, umewatakia wote wanaoshiriki katika mkutano huo, kila mafanikio, na pia amewakumbuka  waandaaji, wasemaji na watazamaji wote  matashi mema na kuwapa baraka zake.

Katika siku hizi tatu za mkutano unatazama zaidi  adhimisho la kupita miaka mitano, tangu 2010 , ya kufanya kumbukumbu ya  miaka mia nne tangu kilipotokea  kifo cha mmisionari Padre Ricci, o wa Macerata. Mkutano unaendeshwa kwa nia kuwakutanisha wanasayansi kutoka China, Ulaya na Marekani, kujadili kwa kina majitolea na mafunzo ya  Ricci , kwa hamu kubwa kutoka kwa   Xu Lin, Rais wa Mkoa wa  Hanban China na Naibu Waziri wa Elimu, ambaye alizindua wazo la kuwa na mkutano huu wakati alipofanya  ziara  rasmi katika chuo cha Confucius cha  Macerata  mwaka 2013. 








All the contents on this site are copyrighted ©.