Jumatatu 19 .10.2015, Wakati wa Mkutano wa kawaida wa Wanahabari kupewa Muhtasari wa Vikao vya Mababa wa Sinodi kwa siku husika, walioshiriki katika kutoa muhtasari huo, pamoja na Padre Federico Lombardi Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Habari ya Vatican, pia walikuwepo wageni waalikwa : Mwenye Heri Patriaki Fouad Twal, wa Upatriaki ya Yerusalemu ya Mashariki, pia Askofu Mkuu Mark Benedict Coleridge, Askofu Mkuu wa Brisbane Australia na Askofu Solmi Henry, Askofu wa Parma. Msgr. Coleridge akiwa pia msemaji wa kundi moja dogo. Na pia Msgr. Solmi hadi hivi karibuni alikuwa Mkuu wa Tume kwa ajili ya huduma ya kichungaji ya familia kwa Baraza la Maaskofu la Italia.
Padre Federico Lombardi alikumbusha adhimisho kubwa la Jumamosi iliyopita ambayo ilikuwa kumbukumbu ya kutimia miaka 50 ya Sinodi ambamo kulitolewa nyaraka mbalimbali za majadiliano na maandiko mbalimbali yaliyokwisha fanyiwa kazi na kutolewa tafasiri katika Kiingereza na Kihispania. Pia kwamba wanasubiri matoleo mengine katika lugha ya kifaransa.
Aidha Padre Federico Lombardi aliwakumbusha wanahabari juu mwaliko wa Mkesha wa Wadomenican wa Jumanne katika nyumba yao ya Mtakatifu Sabina kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 800 ya Shirika la Wadomenicani.
Na kwamba kwa kutoka Ukumbi wa Sinodi kwa Jumatatu asubuhi hapakuwa na michango mipya zaidi. Na hivyo aliwaalika wageni waalikwa kujibu maswali ya wanahabari.
Patriaki Twal, akiizungumzia mikutano ya Sinodi, alilitaja tukio hili kuwa ni jukwaa
linalotafuta kuweka yaliyo mema yote kwa ajili ya familia. Na pia imekuwa ni ishara
nzuri inayoonyesha umoja wa Maaskofu, licha kwamba wametoka mazingira tofauti, na
hivyo kutokuwa na changamoto sawa. Na pia ni jambo la kawaida kuwa na maoni tofauti
katika baadhi ya vipengere na lakini ni wazi hufikia mahali pa wote kukubaliana. Na
kwamba katika kazi za wiki mbili zilizopita, katika kazi ya Sinodi, hapakuwa na kipengere
kilichoachwa bila kuguswa kinachohusu hali ya familia duniani kote. Vikao vilitafuta
njia za kuboresha zaidi maisha ya familia, katika maana ya kibinadamu, kidini na
kama Kanisa zima.
Na kwa upande wa kupokea Ekaristi kwa wanandoa waliopeana talaka na kuoa au kuolewa
tena, kanisa halina jibu moja la ujumla, lakini kila kesi itatazamwa kipekee na kutolewa
jibu kulingana na mazingira ya tatizo la wanandoa husika. Hili ni suala nyeti na
hivyo haliwezi kujumlishwa. Ni lazima kutazama kwa makini msingi wa tatizo, pamoja
na kuwa na hurumani lazima kuzingatia mafundisho ya Kanisa.
Na Askofu Mkuu Coleridge, alilenga zaidi katika kukamilika kwa mkutano wa Sinodi akisema kwamba, majadiliano ya Sinodi hii , si kwamba yanafungwa Jumapili ijayo, lakini yataendelea na safari yake bila ukomo. Na kwamba upana wa mada zinazojadiliwa, ni moja ya sababu kwa nini kumekuwa na changamoto nyingi katika majadiliano.
Naye pia alirejea majadiliano juu ya suala la wanandoa wanaopeana talaka na kuoa au kuolewa tena, kwamba inawapasa Maaskofu si kufikiri katika misingi ya kufikirika, lakini hasa kutazama vizuri mizizi ya hali halisi ya tatizo la kwa kila wanandoa wanaotaka kutalakiana. Na kwamba la muhimu si kuwa na maono ya juu juu matupu, lakini ni lazima kuzingatia uzoefu wa maisha ya binadamu katika taratibu na mapana yake.
Ni lazima kuwa na mazungumzo ya kweli ya kina na wanandoa wenye matatizo. Na hivyo kutokana na mazungumzo ya kweli kwa wanandoa husika, hapo inawezekana kutoa maoni ya kuelimisha kulingana na mafundisho ya Kanisa. Alisema kwamba, Mababa wa Sinodi hawaoni msingi wa kufanya mabadiliko katika mafundisho ya Kanisa. Askofu Mkuu Coleridge, aliendelea kusisitiza kwamba, ni lazima waliooa au kuolewa tena, kuambiwa ukweli na kwa uwazi zaidi masharti ya kurudi katika usharika wa Kanisa, kupokea Ekaristi . Ingawa katika baadhi vikundi vya majadiliano ya kazi za Sinodi, baadhi walitaka uwepo wa kitendo cha huruma kwa wanandoa kama hao, Huruma ya Papa wakati wa Maadhimisho ya Jubilee ya Huruma ya Mungu.
Na Askofu Solmi ameutaja Mkutano huu wa Sinodi kwamba , umeliwezesha Kanisa kupumua
hewa safi ya uzima zaidi kwa Kanisa zima la Ulimwengu. Mkusanyiko huu wa Maaskofu
kutoka pande mbalimbali za Dunia hapa Roma, kujadili masuala ya ndoa na familia katika
hali ya uwazi zaidi, masuala yao, matatizo yao, na hata maadili na mawazo yao kwa
pamoja, umekuwa ni wakati nyeti ambao kwa mara nyingi hasa katika dunia ya nchi za
Magharibi ni suala lililokuwa limesahaulika.
Na ameasa kwamba, majadiliano ya Sinodi hii hayakuwa ya kujipamba kwa "vipodozi”,
lakini ni majadiliano ya kina halisi juu ya Familia kama ni kitovu cha Kanisa na
jamii. Kwa mtazamo wa njia Maungamo yaliyopendekezwa kwa wanaopeana talaka na kuoa
au kuolewa tena, Askofu Solmi, alirudia kutaja umuhimu wa Kanisa kuongozana na wale
walio katika matatizo na zaidi sana wenye kutambua haja ya kuomba msamaha wa Mungu,
wale wanaopenda kujipatanisha tena na Kanisa lenyewe. Hatimaye, alionyesha matumaini
yake kwa matokeo ya Sinodi, kwamba Sinodi hii imefanyika kwa ufahamu kamili wa umuhimu
wa familia kutembea katika njia ya maisha ya Kanisa, wito familia na nafasi yake halali
ndani katika Kanisa. Na ameonyesha matumaini yake kwamba, kwa utambuzi huu hili,
inakuwa ni ishara ya nguvu kwa jamii na taifa zima . Alieleza kwa kuzingatia hasa
mazingira Italia, ambamo mara nyingi anasema, utaratibu wa kijamii umesahau misingi
ya familia.
All the contents on this site are copyrighted ©. |