2015-10-16 14:09:00

FAO yasifu dhamira ya majiji z kupambana na njaa na kuboresha lishe


Tarehe 16 Oktoba ni Siku ya Chakula Duniani, ambayo huadhimishwa chini ya usimamizi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa FAO. Mkurugenzi Mkuu wa FAO, Jose  Graziano da Silva, akizungumza katika  Mkutano wa Kilele wa Mameya juu ya Siku ya Chakula duniani, mkutano uliofanyika  mjini  Milan Italia kwa siku tatu, amesema , majiiji yana  jukumu muhimu katika kufuta  njaa na kuboresha lishe duniani. Na alipokea kwa mikono miwili  dhamira ya majiji zaidi ya 100 duniani, yaliyopania  kuingiza  mifumo ya  chakula ya chakula  katika sera za majiji kwa ajili ya kuleta usawa zaidi na maendeleo endelevu. Da Silva  ametoa shukurani zake za dhati  kwa Meya  Giuliano Pisapia wa Milani na wenzake toka Majiji ya dunia , kwa kusaini Mkataba wa Milan wa Sera ya Chakula.

Pia ametoa shukrani kwa makubaliano majiji , katika kuambatana na kanuni nne, ikiwa ni : kuhakikisha  uwepo wa chakula na afya kwa wote; kukuza  mfumo endelevu wa  chakula; kuelimisha umma juu ya chakula bora, na kupunguza utupaji wa chakula kama taka. Aliendelea kusema watendaji muhimu kwa sera za mafanikio ya maendeleo endelevu yaliyo katika makubaliano ya duniani nzima, ikiwa ni pamoja na kuondoa njaa ifikapo mwaka 2030, ni Mameya , kutokana na ukweli kwamba watu wengi sasa wanaishi vijijini.

Dr Graziano da Silva, aliibaini, lakini ili kufikia malengo haya, Mameya wa Miji  ni lazima waungwe mkono  na sekta zote za maendeleo, tena kwa kipindi kirefu, ikiwemo  pia kushughulikia mabadiliko ya tabia nchi na kupunguza  uzalishaji hasa wa mazao.Alieleza hilo huku akionyesha kutambua kwamba, idadi kubwa ya watu  wanaoishi tayari katika miji,  inatarajiwa kuongezeka, hasa katika nchi zinazoendelea.   Lakini kwa bahati mbaya si miji yote yenye kuwa na  uwezo wa kuhakikisha upatikanaji imara wa chakula na maji kwa wakazi wote wa miji. Na hii inatokana na suala la uhakika wa chakula na lishe  kupuuzwa katika mipango ya miji na maendeleo endelevu, amesema Graziano da Silva.

Mkataba wa Sera ya Chakula wa Milan, ambayo umeandaliwa kwa msaada wa kiufundi na FAO, unatambua umuhimu wa mbinu shirikishi kati ya serikali, sekta binafsi na asasi za kiraia.

Pia  unatambua umuhimu wa kuboresha uhusiano kati ya maeneo ya mijini na maeneo ya jirani ya vijijini. Katika hali hii, Mkurugenzi Mkuu wa FAO,  ametaja  ufumbuzi  bunifu kama vile kutoa msaada wa kuhamasisha ongezeko la idadi ya wakulima wadogowadogo kandokando mwa miji , kama msaada wa kuziba pengo katika upatikanaji wa chakula kutoka maeneo mengine mbalimbali na pia kwa ajili ya uboreshaji wa mlo na afya njema kwa familia zinazoishi  mjini. .

Mkataba wa Sera ya  Chakula ya majiji , umetolewa kama  sehemu ya mipango iliyohusiana na Maonyesho ya Dunia ya Milan Expo 2015,  yaliyofanyika  Milan, chini ya Mandhari "Kulisha Sayari,  Nishati kwa Maisha". FAO  ni kati ya waratibu shiriki wa Umoja wa Mataifa katika Maonyesho ya Expo 2015.  Maonyesho yaliyohudhuriwa na mamilioni ya wageni, wakipata  fursa ya kujifunza zaidi kuhusu masuala yanayohusiana na usalama wa chakula, lishe, endelevu, kupunguza umaskini, maendeleo na ushirikiano, na kazi za Umoja wa Mataifa katika kuwa na dunia isiyo na uso wa njaa.








All the contents on this site are copyrighted ©.