2015-10-14 10:31:00

Bado juhudi makini zaidi zinahitajika kufuta njaa duniani


Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa FAO,  katika taarifa yake ya 2015 juu ya hali ya chakula na kilimo, iliyotolewa kama angalisho kwa Adhimisho la Siku ya Chakula Duniani ambayo huadhimishwa tarehe 16 Oktoba,   inasema , licha ya kupanua hifadhi za kijamii na ufuatiliaji kwa kasi, juhudi za  kukomesha njaa vijijini,bado zinahitajika kuikomboa idadi kubwa ya watu maskini vijijini,  wanaohangaika na uhaba wa chakula na njaa.

Ripoti hiyo ya FAO, inabaini kwamba , leo hii katika nchi maskini , mifumo ya ulinzi wa kijamii,  kama vile uhamisho wa fedha, chakula mashuleni na kazi za umma, hutoa njia za kiuchumi kwa watu hawa maskini wanaoishi katika mazingira magumu, ni fursa ya kuondokana na  umaskini na njaa ,na hivyo kuboresha afya, elimu na nafasi nzuri kwa maisha ya watoto wao. 

Mipango kama  hiyo kwa njia mbalimbali  inaweza kuwa ya manufaa  kwa  watu bilioni 2.1 wa nchi zinazoendelea, ikiwa ni pamoja na kuwaweka watu milioni 150 kutoka katika umaskini uliokithiri.
Kupanua mipango hiyo katika maeneo ya vijijini na kuwaunganisha watu  katika umoja  wa  sera ukuaji wa kilimo, kunaweza leta kasi  katika kupunguza idadi ya watu maskini, inasema ripoti hiyo.

Ripoti hii imetolewa  kama utangulizi kwa ajili ya Siku ya Kimataifa ya Chakula (16 Oktoba), ambayo hulenga kutazamisha watu kwa makini juu ya hali ya  hifadhi za kijamii, kama hatua ya kuvunja  mzunguko wa umaskini vijijini.Mkurugenzi Mkuu wa FAO, Josè  Graziano daSilva anasema , hii ni hoja ya kidharura inayotaka kuungwa mkono , katika kusaidia watu wanaoishi katika mazingira magumu, kuondokana na  adha ya njaa  duniani ..








All the contents on this site are copyrighted ©.