2015-10-05 12:01:00

Mchango wa kwanza wa Papa kwa kikao cha kwanza cha Sinodi


Jumatatu 04 Oktoba 2015,  majira ya asubuhi, katika ukumbi wa Mikutano ya Sinodi wa Vatican, kulianza vikao vya Sinodi ya XIV ya kawaida ya Maaskofu, ikiongozwa na Kauli mbiu: Wito na Utume wa Familia:Ndani ya Kanisa na Ulimwengu mamboleo.  Sinodi hii iliyokutanisha Maaskofu na wajumbe wateuliwa kutoka pande mbalimbali za dunia itaendelea kwa muda wa wiki tatu hadi tarehe 25 Oktoba 2015.

Katika siku yake ya kwanza, ratiba inaonyesha kwamba, Baba Mtakatifu Francisco, anashiriki vikao vya Sinodi mara mbili , asubuhi majira ya saa tatu na pia jioni majira ya saa kumi za jioni.

Katika kikao cha asubuhi, alitoa mchango wake wa kwanza cha  Mkutano  huu, akisema kwa  hakika, jambo hili lilianza muda mrefu kabla,kwa ajili ya  kutathmini na kutafakari  yaliyomo katika rasimu ya kufanyia kazi( Instrumentum Laboris) mada hii: Wito na Utume wa Familia ;Ndani ya Kanisa na Ulimwengu mambo leo ,na utoaji wa fafanuzi juu ya jukumu la sinodi na majibu kutoka Mabaraza ya  Maaskofu na vyombo muhimu husika.

Papa aliendelea kuwakumbusha wajumbe kwamba , sinodi maana yake ni kutembea pamoja,   kwa nia moja na mshikamano, katika ujasiri wa kupitisha yanayotakiwa katika juhudi za kichungaji  na hekima za mafundisho ya kanisa kwa unyofu wa moyo , na daima wakitanguliza mbele yao, yaliyo mazuri kwa manufaa ya kanisa zima, linaloundwa na familia na mwanga unaoongoza Roho za watu.

Kwa mara nyingine Papa aliwakumbusha wajumbe kwamba , Sinodi si mkutano, au kama bunge, au kikao cha Maseneta ambavyo hutafuta kufikia makubaliano. Sinodi,ameitaja kuwa ni jina la Kanisa, linalo maanisha kutembea pamoja katika kuusoma ukweli kwa macho ya imani na kwa moyo wa Kimungu; ni Kanisa linaloingilia kati kwa uaminifu  yale yanayotatiza kwa amana ya imani, na hivyo mikutano yake si kama mahali pa makumbusho ya kutazama ya kale  na wala si mahali tu pa kufanya utetezi, lakini ni  chanzo hai ambamo Kanisa hujinywesha yanayoweza kutuliza kiu ya maisha  na kumulikia katika hifadhi za maisha.

Kwa hiyo Papa anasema, Sinodi ni hatua ya lazima ndani ya Kanisa na katika taifa takatifu la Mungu, ambamo kama wajumbe wa Sinodi, wanatenda kama sehemu ya kazi za ngazi ya juu za wachungaji, au watumishi wa Kanisa. Sinodi pia ni nafasi ya ulinzi wa Kanisa katika kazi za utendaji wa Roho Mtakatifu. Sinodi huongea kupitia maongozi ya Roho kwa  lugha za watu wote wanaoongozwa na Mungu .

Papa alieleza na kuwataka wajumbe wa Sinodi washiriki katika vikao hivi kwa ujasiri wa  Roho Mtakatifu,  ujasiri wa kitume wenye unyenyekevu na maombi  ya Kiinjili bila ya kukatishwa tamaa majaribu ya dunia, yenye kuzima mwanga wa ukweli katika mioyo ya watu. Kuwa na ujasiri wa kitume wenye kuleta maisha  mapya na kuyafanya maisha kuwa makumbusho ya kumbukumbu za Kikristo, kwa unyenyekevu wa Kiinjili.

Papa alieleza na kuwasihi wajumbe pia wasikilize kwa ujasiri na makini, hisia za ndani ya moyo  wakati wanapo jifunua kwa Mungu, katika ukimya wa sala na hisia zao zote , kuisikiliza  sauti ya upole wa Mungu, inayoongea kimya kimya ndani mwao. Papa ameonya , bila kusikiliza sauti ya  Mungu, maneno yao yote yatakuwa ni porojo tupu zisizo kuwa na maana .  Bila kuongozwa na Roho, maamuzi yao yote ni mapenzi ya kidunia ambayo yatalenga,  badala ya kuinua Injili,  yataifunika na kuificha.

Na mwisho, alitoa shukurani zake kwa Kardinali Lorenzo Baldisseri, Katibu Mkuu wa Sinodi na wote anaosaidiana nao, Marais wajumbe, waandishi, washauri, watafsiri na wale wote ambao wanashiriki katika kazi za mkutano huu kwa uaminifu kweli na kujitolea kwa   Kanisa. Na kwamba wanaianza  safari kwa kuomba msaada wa Roho Mtakatifu na maombezi ya Familia Takatifu  ya  Yesu, Mariamu na Yusufu. Asante sana Papa alimalizia.

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.