2015-10-04 13:57:00

Papa wakati wa sala ya malaika wa Bwana


Baba Mtakatifu Francisco kabla ya kusali  sala ya Malaika wa Bwana , Jumapili hii , hotuba yake fupi  iliwakumbuka watoto wengi walio katika mateso ya kuvikimbia vita katika maeneo yao ambao kwa sasa wanapiga hodi katika milango yetu wakiomba msaada na kupokewa.  Aidha alipeleka mawazo ya waliokuwa wakimsikiliza  kwa Sinodi ya Maaskofu ya XIV, kuhakikisha "dhamira ya kutosha kwa ajili ya familia na jamii. Aidha aliomba sala za waamini  ili dunia iweze kuwekwa huru dhidi ya vita, na pia aliwakumbuka kafara wa maporomoko ya aridhi huko Guatemala na Ufaransa .

Papa alieleza hayo, muda mfupi kupita baada ya kuongoza Ibada ya Misa kwa ajili ya kufungua Mkutano wa Sinodi ya Kawaida ya Maaskofu wa XIV, iliyoanza leo 4 Octoba na kuendelea hadi 25 Oktoba 2015.  Alitaja nia ya Sinodi hiyo akisema kuwa ,
Mababa wa Sinodi, waliotoka kila sehemu ya dunia na kukusanyika karibu mwandamizi wa Petro, kwa muda wa wiki tatu, watatafakari juu ya “Wito na utume wa  familia, katika Kanisa na katika jamii, kwa utambuzi makini wa kiroho na Kichungaji”.  

Papa amesema, katika wiki hizi tatu,  wanayakaza macho yao kwa Yesu, ili kupata, misingi ya mafundisho ya Yesu ya kweli na huruma yake  katika njia  sahihi zaidi, kwa dhamira ya kutosha ya Kanisa na familia na kwa ajili ya familia zote, ili kwamba mpango asili wa Muumbaji  kwa mwanamume na mwanamke uweze tekelezwa kupitia kazi yake nzuri na nguvu yake katika dunia ya leo.

Papa alieleza kwa kurejea liturujia ya Neno ya Jumapili hii , ambayo maandishi yake yana msingi  wa mwanzo katika kusaidiana na usawa kati ya mwanamke na mwanaume (Mwa 2.18-24). Papa alieleza na kunukuu maneno ya  Biblia yanayosema  kwa ajili hii  mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ataungana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. Alifafanua kuwa  ni maisha ya watu wawili  ambayo kwa sakramenti ya ndoa yanaungana na kuwa kitu  kimoja na sawa. Na hivyo wanandoa katika usawa huo wanapokea jukumu la kuendeleza maisha ya binadamu mpya kama wazazi. Kushiriki katika ubunifu na nguvu za uumbaji za Mungu mwenyewe. Lakini pia wanatakiwa kuwa makini! Mungu ambaye ni upendo, anaichukua  sehemu ya kazi  yake nyeti yake ya uumbaji, na kuidhaminisha kwa viumbe katika hali ya  upendo pamoja naye na kama Yeye .

Kwa maana hii -. Kama Mtakatifu Paulo anavyosema - upendo amekwisha miminwa mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu tuliyepewa sisi (Rum 5 , 5). Na hii pia ni upendo ambao unatolewa kwa wanandoa katika sakramenti ya ndoa. Papa alieleza na kusema, ni  upendo ule ule, katika Injili ya leo, Yesu anaonyesha kwa watoto: "Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana wao ni warithi wa  kweli wa Mungu wao" (Marko 10:14).

Papa aliendelea kueleza kwamba, wakati huo walikuwa wakitolea maombi kwa  Bwana, ili kwamba, wazazi wote na walimu kama pia ilivyo jamii yote duniani, awafanye wote kuwa chombo cha kuwapokea  kwa  upendo ulio unadhihirisha na Yesu kwa watoto wadogo. Yeye huonekana ndani ya nyoyo zenye huruma na wasiwasi kwa baba na mama, wanaopata kwa wakati mmoja juu ya watoto wao . Papa kwa mawazo hayo , alionyesha kuguswa na mahangaiko na mateso ya watoto wengi wenye njaa au waliotelekezwa , wanaodhulumika , au kulazimishwa kufanya kazi za kijeshi kama wapiganaji au wapagazi, na hata wale wanakataliwa na familia zao kutokana na hali zao za udhaifu wa mwili n.k . Alisema hujawa na simanzi na uchungu mkali, pale anapotazama picha za watoto waliojaa uchungu , ambao wako katika harakati za kukimbia umaskini na migogoro, wenye  kugonga kwenye milango yetu na mioyo yetu, wakiomba msaada. Papa alimwomba Bwana, atusaidie sisi kutokuwa ngome ya nguvu ya ukatili wa jamii, bali tuwe familia na jamii yenye uwezo wa kuwapokea wote kwa mujibu wa sheria sahihi.

Papa alikamilisha hotuba yake kwa kuomba sala za waamini zisindikize kazi za Sinodi, ili kwamba Roho Mtakatifu afanye kazi yake ndani ya mioyo ya Mababa wa Sinodi kikamilifu na kwa utulivu na maongozi yake. Na aliomba maombezi  Mzazi wa Yesu, Bikira Maria, kuungana na wote kiroho, ambao, kwa wakati huu, wamekusanyika katika Madhabahu ya Mama yetu wa Pompeii, kuomba neema na baraka kwa Mama yetu wa Rozari.

Baada ya sala ya Malaika wa Bwana,  Papa alikumbuka tukio la kutajwa kuwa Wenye Heri huko  Santander, Hispania, Mtumishi wa Mungu Padre  Pio Heredia na wenzake kumi na saba wanashirika wa  Cistercian wa Mtakatifu Bernardo, waliouawa kwa  kukataa kuikana imani yao wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Hispania na mateso ya kidini katika wakati wao.  Papa alisema “Tunamsifu Bwana kwa  ujasiri wa mashahidi hawa, na hivyo tunaomba  maombezi yao,  na kuyaweka kwa unyenyekevu  majanga yote ya vita yanayotokea hata kwa nyakati hizi”. Na aliwashukuru wote waliotoka maeneo mbalimbali kwa ajili ya kushiriki katika Ibada hii. Na kwa ajili ya  Siku ya Mtakatifu Francis wa Assisi, Mtakatifu mlinzi wa Italia. Kwao wote aliwapa salaam zake za upendo, na kuwaomba wasimsahau katika sala zao. 








All the contents on this site are copyrighted ©.