2015-09-21 10:11:00

Papa Francis awahimiza vijana wa Cuba kuwa na matumaini hai


Jumapili, Baba Mtakatifu baada ya sala ya masifu ya jioni alikutana na umati mkubwa wa vijana waliokuwa wanamsubiri kwa hamu katika Kituo cha Utamaduni cha Padre Felix Varela cha mjini Havana.

Mahali hapo, Papa Francisco aliwahimiza vijana kuishi kwa  matumaini wakijenga mshikamano na mapenzi ya kukutana na wengine . Kituo hicho  kilichoanzishwa   mwaka 2011 na Jimbo Kuu la Havana kwa msaada wa Baraza la Kipapa kwa Utamaduni, hufundisha masomo ya theolojia, falsafa, sosholojia, saikolojia na utawala wa biashara. Pia kuna kumbi za mikutano, tamasha na  maonyesho yanayofanywa kwa ushirikiano  na wadhamini wa   tamasha la filamu la Amerika ya Kusini.

Papa baada ya kusikiliza hotuba nzuri ya Mkuu wa kituo hicho na risala ya mwanafunzi  kijana, aliyependa kumshirikisha Papa mawazo ya vijana katika matumaini yao kwa mustakabali wa nchi yao, Papa,  alijibu risala hiyo, kwa kuwahamasisha vijana , waweka hai ndoto zao kwa kuzingatia zaidi mambo yanayolenga kujenga mshikamano , kuliko mambo yanayowatenganisha.

Papa pia alizungumzia juu ya tatizo la ajira kwa vijana na haja ya vijana kujijenga  katika utamaduni wa kukutana, na kuwataka wanafunzi kuweka mioyo yao na akili  yao wazi, badala ya kuyafungia waliyo nayo ndani  yao wenyewe.

Aidha katika hotuba yake aliyokuwa ameiandaa tayari, Papa alishirikishana mawazo na wanafunzi katika mtazamo wa  kutafuta njia ya matumaini katika maisha yao, akitaja njia tatu,  kwanza, ikiwa ni kudumisha  kumbukumbu ya urithi wao wa kiroho na kimaadili. Pili, ni kusafiri pamoja katika njia ya maisha na wengine na tatu ni kuonyesha mshikamano kwa ajili ya ustawi wa taifa kwa siku za baadaye .  

Baba Mtakatifu alieleza kwamba, njia ya maisha humulikiwa na matumaini , tumaini linalotokana na imani kwa Kristo. Yesu, Mwana wa Mungu alishuka yeye mwenyewe na kuandamana nasi katika njia hii ya maisha. Na si tu hututia ujasiri sisi , lakini huandamana nasi , akiwa ametushika mkono . Mwana wa Mungu , aliyetaka kuwa kama sisi wenyewe, huandamana nasi katika Na kwa kuwa naye katika maisha yetu , tunajifunza jinsi kuona ukweli , kwa kukutana na kuwahudumia wengine na kutembea pamoja katika njia ya umoja na mshikamano. 








All the contents on this site are copyrighted ©.