Taarifa kutoka Vatican zinasema Jumapili 28 Agosti Monsinyo Pierfracon Pastore aliyekuwa na umri wa miaka 88 amefariki dunia.
Askofu Pastore aliwahi kuwa Katibu wa Baraza la kipapa katika Mawasiliano, na kufanya kazi radio Vatican kwa miaka mingi.
Tangu 2003 alikwenda pensheni lakini aliendelea kuwa mshauri mwema kwa waandishi wa habari na wahudumu wa vyombo vya mawasiliano kila mara walipokuwa wanahitaji msaada wake.
Ibada ya mazishi itafanyika Roma Jumanne 1 Septemba kwenye Kanisa liloko katika kituo cha Umoja wa vijana Katoliki kabla ya kusafirishwa mwili kwenda Novara Italia.
All the contents on this site are copyrighted ©. |