2015-08-25 07:41:00

Maaskofu wa Uganda wamuenzi Marehemu Askofu Kalanda


Mwenyekiti wa Baraza la  Maaskofu Katoliki Uganda  (UEC) ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Gulu, Askofu Mkuu  John Baptist Odama, amemwelezea  Marehemu  Askofu Paul Kalanda, Askofu Mstaafu wa Jimbo Katoliki la Fort Portal, kwamba alikuwa ni mtu muhimu, mshauri mkubwa, mmisionari na nembo ya hekima. Maelezo ya Askofu Mkuu Odama yalifuatia taarifa za kifo cha Askofu Kalanda, aliyefariki katika usingizi, asubuhi ya  Jumanne iliyopita Agosti 18,  katika makazi yake ya Villa Maria, Jimbo la  Masaka, Uganda.

Askofu Mkuu Odama akirejea taarifa za kifo cha Askofu Kalanda, amesema, alizipokea kwa huzuni kubwa, kwa kuondoka kwa Mtendaji mkuu huyu wa Kanisa aliyempenda Kristo na kanisa lake bila kujibakiza. Na kwamba, wakati Askofu Kalanda akiwa  Mwenyekiti wa UEC, alitumikia kwa upendo sio tu kwa Kanisa lakini kwa taifa zima la Uganda. Ni mtu aliyependa  umoja, amani na maendeleo kwa taifa lake la Uganda. Na hivyo Kanisa limepoteza  mmoja wa watu wake mashuhuri, jasiri na muhimu. Mchango wake ulikuwa bado unahitajika hasa kwa wakati huu wa mchakato wa  mabadiliko nchi Uganda.

Askofu Paulo Kaloanda  alizaliwa Februari 24, 1927 katika kijiji cha Buwunde, Jimboni  Masaka , kwa familia  Baba Simon Zilyawukanya Kalanda na Mama Agnes Nakachwa , akiwa mmoja wa watoto watano, wavulana wanne na binti mmoja.

Baada ya kuhitimu masomo kwa ajili ya Upadre, alipadrishwa Desemba 21, 1957 na baada ya hapo aliendelea na masomo yake katika Chuo Kikuu Kipapa cha Gregorian cha mjini Roma ambako alipata Shahada ya Uzamivu katika  falsafa (PhD) ya sheria za Kanisa mwaka 1961.Na baada ya hapo kurudi nchini mwake kulitumikia Kanisa. 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.