2015-08-20 09:05:00

Kongamano la Misitu la Dunia la XIV Durban


Mtazamo wa 2050 kwa misitu na hali zake – Ni mada itakayozindua Tathmini ya Dunia juu ya Rasilimali za  Misitu  2015

Haja ya serikali, asasi za kiraia na sekta binafsi kuongeza uwekezaji katika misitu, itakuwa ni kipengere muhimu kwa maendeleo endelevu  katika Kongamano la Dunia la  XIV la  Misitu litakalo fanyika Durban, Afrika Kusini, kuanzia Septemba 07-11 mwaka 2015.

Kongamano linaongozwa na Madambiu ; Misitu  na Watu: Uwekezaji katika mstakabali wa  Maendeleo endelevu ,ambamo  washiriki watajadili njia za kuongeza uwezo kamili wa misitu na kuinua ustawi wa wakazi vijijini, kujinasua na umaskini, kama kitendo pia  cha kukabiliana na  mabadiliko ya tabia nchi na uhamasishaji wa  teknolojia mpya na bidhaa mbadala.

Mawaziri na wakuu wa vyombo vya kitaifa na kimataifa watakuwa kati ya washiriki wa Kongamano hili litakalo jumuisha pamoja maelfu kadhaa ya watu katika kongamano hili lenye kufanyika kila baada ya  miaka sita. Kongamano la mwaka huu linafanyika mjini Durban Afrika Kusini,  kwa msaada wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika Afrika, tangu kuanzishwa kwake mwaka 1926.

FAO, inataarifu kwamba, kati ya mambo muhimu yatakayo fanyika ni pamoja na  uzinduzi wa Tathmini ya Dunia ya Rasilimali ya Misitu 2015, ambayo itaonyesha jinsi misitu ya dunia nzima  ilivyo badilika katika kipindi cha miaka 25 iliyopita na kutoa taarifa za karibuni juu ya hali ya usimamizi endelevu wa misitu.

Matokeo Kongamano hili  la Matazamio ya 2050, yanatarajiwa kupendekeza uwezo wa  kuimarisha mchango wa misitu na uoto wake kwa mustakabali endelevu na kusaidia kusafisha barabara kwa ajili ya protokali  mpya juu ya  mabadiliko ya tabianchi, inayotazamiwa kupitishwa  katika Mkutano wa Nchi  Wanachama wa Umoja wa Mataifa juu ya Mabadiliko ya Tabianchi, katika Mkutano wa Kilele utakao fanyika mjini Paris  Desemba, 2015.

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.