2015-08-15 09:58:00

Vatican na Timor ya Mashariki watia saini Mkataba wa ushirikiano


(Vatican Radio) Kardinali Pietro Parolin, na Waziri Mkuu Rui  Maria de Araujo,  Ijumaa (14 Agosti) waliweka saini katika hati ya makubaliano ya kushirikiana katika masuala ya uhusiano wa  kisheria kati ya Jimbo Takatifu na Jamhuri ya Timor ya Mashariki. Akizungumza katika hotuba baada ya kusaini mkataba huo, Kardinali Parolin, aliitaja hati waliyoweka saini kuwa ni ishara kubwa ya matunda ya mahusiano mazuri kati ya Kanisa Katoliki  na Serikali ya Timor ya Mashariki. Uwekaji wa sahihi huu umekuwa ni moja ya matukio makubwa  katika maadhimisho ya kupita miaka mia tano,  tangu Neno la Injili lilipohubiriwa kwa mara kwanza Timor ya Mashariki.  Kardinali Parolin aliteuliwa na Papa Francisco kumwakilisha katika maadhimisho haya.

Utiaji wa sahihi katika hati ya makubaliano ya ushirikiano na mshikamano wa kisheria, ulihudhuriwa pia na Rais  Taur Matan Ruak,  wa Jamhuri ya Timor ya Mashariki;  Vicente Guterres, Rais wa Bunge la Taifa; na Rais wa Mahakama ya Rufaa ,  Guilhermino da Silva, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje Hernani Coelho, pamoja na kundi la wabunge na maofisa wa ngazi ya juu serikali, wanadiplomasia, Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa na Maaskofu wa Timor ya Mashariki.

Kardinali Parolin akitoa neno baada ya utiaji wa saini, alishukuru kwa kupata upendeleo huo wa kuweka saini katika hati hiyo muhimu  ya Mkataba kati ya Jimbo Takatifu na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Timor ya Mashariki. Mkataba, wa kisheria utakao tumika kama chombo cha kuongoza uhusiano kati ya Kanisa Katoliki na Serikali ya Timor ya Mashariki,  katika masuala  msingi  kwa ajili ya  watu wapendwa wa Timor- Mashariki.  Aliitaja hati hiyo kwamba ina lengo moja tu  kuu nalo ni  kuwa na namna bora ya kusaidia watu kufanikisha maendeleo endelevu kwa  jumla, kimwili na kiroho.

Kardinali Parolin, alikumbusha kwamba, wote Kanisa na Serikali, uwepo wake ni  ajili ya kutumikia watu , na hivyo kwa Mkataba huu waliotia saini,  unakuwa uthibitisho unaodai uwajibikaji katika kuwatumikia watu kwa mujibu wa yaliyoandikwa katika mkataba huo, maandishi yanayodai kushirikiana na kuheshimiana kwa  ajili ya maendeleo kamili ya watu katika haki, amani na manufaa ya wote.

Na alirejea uzoefu wa siku za nyuma , akisema daima umeonyesha, binadamu hupata huduma iliyo bora zaidi pale kunapokuwa na ushirikiano na mazungumzo kati ya sehemu zote za jamii na pale  panapojengeka utamaduni imara wa kukutana kwa amani na kuheshimiana, na hasa miongoni mwa viongozi.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.