2015-08-13 07:50:00

Papa achagua kauli mbiu ya Siku ya Kuombea Amani Duniani 2016



Baba Mtakatifu Francisko kwa  ajili ya maadhimisho ya Siku 49  ya Kuombea Amani Duniani, 2016, ametangaza kauli mbiu ya ujumbe kuwa : kushinda tofauti na kushinda amani. Ujumbe unalenga kuondokana na roho ya ubaguzi wa kujiona kuwa tofauti na mwingine badala yake pamoja na utofauti iwe kujenga moyo wa amani na wote bila kujali tofauti zilizopo.  Hii ni mara ya tatu kwa Papa Francisco kutoa ujumbe wake kwa siku hii ya Dunia ya kuombea amani tangu alipochaguliwa kuwa Papa.  Papa anaona kwamba, katika wakati huu wetu, hali ya kujali tofauti ni moja ya sababu za msingi za ukosefu wa amani.  Anasema hii tukitazama kwa kina, kutofautiana  mara nyingi,  imekuwa ni chimbuko la aina mbalimbali ya ubinafsi, ikisababisha kujitenga, ujinga, na ubinafsi, kunako leta ukosefu wa uwajibikaji na upendo kwa watu wengine.

Aidha Baba Mtakatifu Francisko anasema, wingi wa habari zinazotolewa juu ya maovu mbalimbali yanayofanyika duniani, haimanishi uwepo pia wa juhudi nyingi zinazotafuta kutatua matatizo na changamoto zilizopo, na hasa  iwapo habari hizo hazitasaidia kuleta moyo wa mshikamano uliosimikwa katika misingi ya dhamiri na uwazi .  Kwa maana hii, ni muhimu habari iwe kwa ajili ya kuchangia uelimishaji si tu kwa familia, lakini kwa makundi mbalimbali ya kijamii, walimu, waandishi wa habari, wasomi na wasanii...hasa juu ya kila mmoja kuishi kwa uhuru wa dhamiri yake bila kujali tofauti yake na wengine maana kwa kufanya hivyo huleta ushindi katika kukabiliana na kishawishi cha kutaka kubagua wengine na kujitenga. 

Baraza la Kipapa kwa ajili ya haki na amani, likieleza juu ya Kaulimbiu ya ujumbe wa Papa kwa Siku ya Kuombea Amani Duninai 2016, linasema  Papa Francisko  analenga kusisitiza kwamba, amani haiwezi kupatikana bila Juhudi, au  bila ya kuwa na uongofu kiakili na kiroho, au  bila hisia ya ubunifu na ushirikiano katika majadiliano, kwa faida ya wote.

Kuna hitaji la watu kubadilika kifikra, tena dhatri muhimu na la kidharura, kwa ajili ya kujenga hisia za uwajibikaji wa kutambua  matatizo makubwa na changamoto za  wakati wetu, kama vile, itikadi kali za  kutovumilia wengine, kutoona kama kuua na kutesa wengine kwa sababu ya imani na ukabila, kutokuzingatia uhuru na uharibifu wa haki za watu wote, unyonyaji wa binadamu na mbalimbali za utumwa, rushwa na uhalifu wa kupangwa, vita na hatma ya wakimbizi na watu waliolazimishwa kukimbia makazi yao. Mabadiliko ya moyo  na uwajibikaji, haina maana ya kubadili dini au imani kwa kuwa dini na imani zote za kweli,  hudai uadilifu, haki na amani.  HIvyo mageuzi ya kuwa watu adilifu, ni fursa na uwezekano wa kupambana na maovu hayo kwa kuunda  utamaduni  wa sheria, ufahamu katika umuhimu wa uwepo wa majadiliano kwa ajili ya kubadilishana maoni na ushirikiano. Kwa  mtazamo huo, pamoja unakuwa ni ujenzi wa  msingi thabiti katika  kukabiliana na matatizo na changamoto zinazojitokeza.

Baraza la Kipapa  linakumbusha pia kwamba, Ujumbe wa Papa wa kwa ajili ya Siku ya  Kuombea Amani Dunia kwa mwaka huu 2015, pia ulihimiza ujenzi wa amani kwa maisha ya  kila siku , kwa ajili ya kuzishinda changamoto za utofauti, uliosimiskwa katika mifumo mbalimbali  ya utumwa mambo leo. Ujumbe uliotolewa chini ya Mada Mbiu: Hakuna tena watumwa bali sote ni ndugu kaka na dada. Hivyo tunapaswa kuendelea kujenga  uadilifu na ushirikiano.
Ujumbe unaendelea kusema, Amani huiwezi kuwepo bila haki ya kila binadamu kutambuliwa na kuheshimiwa kwa mujibu wa uhuru kamili na haki. Ujumbe kwa  mwaka 2016 unalenga kuwa mahali pa kuanzia watu wote wenye mapenzi mema, hasa wale wanaofanya kazi katika elimu, vyombo vya habari, utamaduni, na kila mmoja kutenda kwa jinsi inavyotakiwa  kwa mujibu wa uvuvio na matazamio ya kujenga umoja na ushirikiano na hivyo kuwa na dunia iliyo na huru na haki.

Siku ya Kimataifa ya Kuombea  Amani Duniani, ilianzishwa na Papa  Paulo VI, kwa kila siku ya kwanza ya mwaka mpya  yaani Januari Mosi. Ujumbe Baba Mtakatifu kwa ajili hiyo, hutumwa kwa  Mawaziri wote wanaohusika na Masuala ya nchi za nje duniani, na pia ujumbe huonyesha mwelekeo wa utendaji wa shughuli za kidiplomasia kwa Jimbo la Papa katika kipindi cha mwaka mzima. 








All the contents on this site are copyrighted ©.