2015-07-21 15:34:00

Papa :Mchungaji mwema hukaa karibu na kondoo wake.


Adhimisho la miaka mia tano, alipozaliwa  Mtakatifu Philipo Neri, linakumbusha kwamba mchungaji mwema hukaa karibu na kondoo wake.  Ni ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisco, kwa ajili adhimisho la miaka mia tano ya kuzaliwa Philipo Neri , hapo tarehe 21 Julai 1515.   

Mama Kanisa, hasa kwa namna ya kipekee katika Jimbo la Roma, Jumanne hii, ameadhimisha Siku kuu ya kuzaliwa Mtakatifu Philip  Neri , Mtakatifu Maarufu  aliyezaliwa Florence  Italia, 21 Julai 1515, na baadaye kuhamia Roma,  ambako alikuwa na maisha kustajabisha,  yenye upendo mkuu  kwa  watu maskini zaidi.

Papa Francisco anasema ingawa zimepita karne tano , kumbukumbu za uwepo wake zinaendelea kuwa hai miongo mwa watu wa Roma, , hasa kwa jinsi alivyoishi kwa mshikamano na kwa furaha kubwa na  maskini na  leo anaendelea kuwa harufu nzuri inayovutia  kutumikia maskini, kama inavyo endelezwa na Shirika lake la Mtakatifu  Philipo Neri .

 Kwa ajili ya Siku Kuu hii, Papa Francisco kwa  roho ya Kibaba, hapo Mei  26 alipeleka barua kwa Shirika la Mtakatifu Phillipo  Neri , kwa ajili ya kuadhimisha  miaka mia tano tangu kuzaliwa Philip Neri.

Papa katika Ujumbe wake,  ameonyesha kutambua jinsi Mitume  Petro na Paulo, na Philip, wanavyo  tambuliwa na kuheshimiwa kama Mitume watatu wa Roma, kutokana na mapenzi yao kwa watu wa Roma.  Wakazi wa Roma husema ,  Philip Neri ingawa alizaliwa wa  Florence,  alizaliwa upya  Rome, kwa ajili ya watu wa Roma.  Papa amerejea maelezo ya kihistoria yanayosema, alifahamika kote katika maeneo ya wazi ya jiji na katika vichochoro vya  Roma, ambako waliishi watu maskini  zaidi.   Philipo aliwatembelea watu hao  kama mchungaji Mwema bila ya kujali  hali yao duni,  yeye aliisikia harufu ya kondoo  na siyo  harufu mbaya ya maradhi na umaskini. Aliwafariji  kwa  utajiri wake wa kiroho.

Ujumbe wa Papa Francisco unaendelea kuyakumbuka maisha ya ukarimu na upendo wa Mtakatifu Philipo Neri, hasa kwa jinsi alivyo kuwa pia na mapenzi ya  Neno la Mungu .  Papa anasema hii  ilikuwa ni siri yake iliyompa nguvu na ujasiri wa roho. Ubaba wake wa kiroho, anaendelea  kusema Papa Francisko, uliangazia mapito ya kazi yake yote, sifa na uaminifu kwa  watu na katika furaha ya  uongofu unaotokana na imani thabiti ,  neema isiyoondoa asili, lakini hujaza  nguvu na ukamilifu.  Ndiyo yeye aliwaendea waliokuwa dhaifu na kuwapa kidogo alichokuwa nacho,  na wote walimkaribia na kuwa marafiki zake, Maelezo binafsi ya  Mtakatifu Philipo Neri yanasema.  Na kwamba, kwa hiari alitenda na kujikatalia mambo ya mpito ya kidunia, akipendelea  zaidi kujifurahisha na kujielimisha na fadhila za  Ukristo ,  wakati huo huo, akiwa mtu wa  nidhamu na mapenzi makubwa  katika utume wake na katika  kumkubali Kristo kama  ukweli wa maisha yake. .

Papa Francisco ameeleza na kutoa Shukrani zake za dhati kwa  utume wa Mtakatifu Philip, akionyesha pia kutambua  ahadi ya wokovu wa roho  kuwa kipaumbele kwa ajili ya Kanisa, akisema, hii ndiyo njia,  wanayo paswa kutembea ndani yake wachungaji  wote wa Kiroho, katika kuwaongoza  na kusaidia watu kufikia ukomavu wa imani yao.  Kuwa mchungaji mwenye ni kuitoa  nafsi kwa ajili ya wengine, kama Philipo , ambaye mwaka  1551, alijiunga katika daraja la ukuhani bila kubadilisha mtindo wa  maisha yake. Katika  kumbukumbu za nyakati, sura yake haijafutika machoni pa jamii. Kutokana na mapenzi yake kwa jamii iliyokuwa mzunguka, iliundwa  jumuiya ya kwanza kwa karama za sura yake ,  ambayo  mwaka  1575 ilipokelewa kwa  ridhaa ya Papa Gregory XIII.

Padre Philipo Neri , anaendelea kukumbukwa, jinsi  daima alihimiza waamini , kuwa wanyenyekevu, kujishusha chini kwa unyenyekevu, kama watoto wa Mungu. Aliwaonya kwamba, katika kuwa watoto wa Mungu "haitoshi kuwa watu wa kuheshimu yaliyo ya juu peke yake  lakini pia ku heshimu yote yaliyoumbwa na Mungu.

Papa Francisco ameutaja huo kuwa ndiyo wosia  msingi wa Mtakatifu Philip, kuwa na unyenyekevu kama  wa mama Bikira Maria alivyokuwa miguuni pa Yesu.

Mtakatifu Philip Neri , Mtume wa tatu wa Roma,  alifumba macho yake  daima Mei 26, 1595. Lakini upendo wake kwamwe haujazima  katika mioyo ya watu Roma, ambao kwa wakati huu Papa Francisko anatumaini wanajiandaa vyema pia kwa ajili ya  Jubilee ya Huruma ya Mungu. Anasema huu si muda wa kulala, kwa kuwa  Paradiso haikujengwa kwa  ajili ya wazembe. 








All the contents on this site are copyrighted ©.