2015-07-19 12:00:00

Papa asema: kuona , kuwa huruma na kufundisha, ni maneno ya mchungaji


Papa Francisko  ametaja maneno matatu : kutazama , huruma na kufundisha kuwa tabia  ya kiongozi yoyote mwema.  Papa  alieleza hilo wakati wa sala ya Malaika wa Bwana akiwa hapa Vatican, ambako makumi ya maelfu ya watu walikusanyika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, majira ya adhuhuri kumsikiliza licha ya jua kali.

Hotuba ya Papa ililenga katika somo la Injili ya Jumapili hii ambamo mnaeleza  kwamba,  Mitume, baada ya kufanya kazi nyingi kwa  furaha lakini pia walionekana kuwa na uchovu, wakihitaji kupumzika kidogo kando faraghani, mbali na makundi ya watu  na Yesu alitambua hilo. Lakini watu walivyoona  hivyo, waliwatangulia mbele yao. Yesu aliwatazama watu hao na kuwahurumia  akiwaona kama wanakondoo wasiokuwa na mchungaji,  hivyo alianza kuwa fundisha mambo mengi( Rej. Mk6,31-34).

Baba Mtakatifu Francisko anasema katika  somo hili,  tunajifunza mambo matatu : kuona kwa makini, kuwa na huruma na kufundisha. Mambo haya , ni sifa ya kiongozi au mchungaji mwema.  Papa anafafanua  sifa ya  kwanza na ya pili, katika mtazamo wa mahusiano yake na  Yesu,akisemani kutazama mambo kwa makini si kama  mtalaam wa sosholojia au  mwanahabari au  mpiga picha, lakini ni kutazama katika kina cha moyo,mtazamo wa "macho ya kiroho".  Hivi vitenzi viwili,kuona na huruma, ni sifa ya  mchungaji mwema kama  Yesu  alivyo.  Papa aliendelea kutazama kwa kina huruma ya Yesu akisema,  haikuwa hisia za kibinadamu, lakini hisia halisi za Masiya aliye  alifanyika mwili, ambaye ni  huruma ya Mungu. Na huruma hii, ilimpa Yesu  hamu ya  kulisha umati kwa chakula cha Neno lake kwa kufundisha.

Baada ya kutafakari ujumbe wa Injili, Papa pia aliutumia wakati huu wa sala ya Malaika wa Bwana  kutoa shukurani zake kwa  Roho wa Yesu, Mchungaji Mwema, kwa kumwongoza  wakati wote wa ziara yake ya  kitume ya zaidi ya wiki, kutembelea Mataifa matatu ya Amerika ya Kusini Ecuador, Bolivia na Paraguay hivi karibuni.  Mbele ya mahujaji na wageni, Papa kwa dhati amemshukuru Mungu  kwa ajili ya zawadi hii. Na pia alirudia kwa mara ingine kutoka shukurani zake kwa mamlaka ya nchi hizo kwa ukarimu wao na ushirikiano. Na kwa upendo mkubwa, amewashukuru tena  ndugu  zake  Maaskofu, mapadre, watawa, walioweka maisha  wakfu na watu wote kwa ajili ya mapokezi mazuri na ushiriki wao.  Kwa ajili hiyo Papa alimtukuza Bwana aliyefanikisha kazi za utume wake kwa  Watu hawa Mungu, walio katika hija ya maisha, wakiwa wamehamasika katika imani na katika utamaduni wao.  Na kwa ajili ya kuwawezesha wote kumtukuza Mungu kwa shukurani  na sifa  kwa  ajili ya mazingira asilia mazuri, yenye utajiri mkubwa nchi hizo.

Papa amekiri kwamba  bara hili la Amerika ya Kusini , lina utajiri mkubwa  wa ubinadamu na uwezo wa kiroho, uliofumbatwa katika thamani ya kina cha  mizizi ya  maadili ya Kikristo, licha pia ya kukabiliwa na matatizo makubwa ya kijamii na kiuchumi. Kwa ajili ya kutoa mchango wake katika kupata  ufumbuzi wa changamoto zinazo wakabili, amesema jukumu la Kanisa, kuendelea  kuhamasisha  tunu za kiroho na kimaadili katika jamii,  kwa kushirikiana na  watendaji  wengine wote kwa ajili ya kujenga ustawi wa jamii nzima..

Na ameonyesha kutambua  jinsi  wanavyokabiliwa na  changamoto kubwa katika kuitangaza  Injili ya Kristo, mbele ya  uso huo,  Papa anatoa mwaliko kwa wote kuteka toka kwa Kristo Bwana neema  zake, kwa kuwa neema za Bwana zina nguvu kubwa ya kuokoa na ni nguvu ya dhamira ya  kumshuhudia  Kikristo, katika kukuza usambazaji wa Neno la Mungu, hadi roho wa kidini aweze  kuwa  nguvu zaidi kwa   watu wote, na katika kuwa   daima  shahidi  aminifu wa Injili.

Papa Francisco alieleza na kuomba maombezi ya Mama  Yetu Maria wa Guadalupe, , ili kwamba,  wote wa Amerika ya Kusini, waweze kuheshimu kuwa chini ya Msimamizi wao Mama Yetu wa Guadalupe.  Pia  Papa ameyakabidhi matunda yote ya ziara yake  ya kitume Amerikaya Kusini, katika Usimamizi wa Maria, na ameitaja ziara hiyo kwamba hataisahau.








All the contents on this site are copyrighted ©.