2015-05-14 09:47:00

Caritas popote yahimizwa kutopoteza utambulisho wake wa kikanisa


Askofu Giampietro Dal Toso , Katibu wa Baraza la Kipapa  kwa ajili ya utoaji wa misaada ya Jimbo la Papa  kwa wahitaji, Baraza  linalojulikana kwa jina "Cor Unum” akishiriki katika Mkutano Mkuu wa  XX wa Taasisi ya Kimataifa ya Misaada Katoliki, ” Caritas Internationalis”,  ameshukuru uwepo  wa taasisi hiyo kimataifa, yenye kuvuviwa na  upendo wa kiinjili katika juhudi zake  za utetezi wa haki na ustawi wa wote. pamoja na hilo, amesisitiza umuhimu wa kutunza utambulisho na kanuni zinazoongoza Caritas mahali popote duniani.

Askofu Toso, kwa namna ya pekee ametaja umuhimu wa dhana ya ushirikiano,  kama chimbuko la nguvu zote za utendaji wa Caritas , kati ya ngazi ya Kimataifa na matawi yake yote ya  pembezoni. Alisema , kwa kweli, dhana ya ushirikiano ndani ya Caritas, umethibitisha  ukweli kwamba, inawezekana  kuwa na vyombo mbalimbali vya kujitegemea, kutenda majukumu yake ya kawaida kwa kushirikiana na wengine.  Na  ushirikiano huo,  hauna maana ya kuondoa uhuru wa kila mmoja .  Hivyo, unakuwa si mfumo unaofungwa na uwepo wa serikali moja kuu,  lakini ni kinyume chake , kila  Ofisi yake kijimbo, na kitaifa hufanya azi zake  kwa kujitegemea lakini katika utendaji wenye mshikamano  wa pamoja na nchi zingine, katika kukabiliana  matatizo yanayofanana..  Kanuni hii , ndiyo nguzo muhimu ya kuuelewa muundo wa  Shirika la kimataifa la Caritas Internationalis  na wanachama wake kitaifa.

Mons. Tosso aliendelea kuzitazama hali halisi za nyakati hizi  na kushukuru kwamba,  kuna ushirikiano thabiti kati ya Caritas Intenationalis  na huduma za Caritas katika Majimbo, utendaji unaoonyesha uimara wa chombo hiki katika utumishi wa upendo wa  Kanisa katika ngazi ya  kimataifa na kitaifa , ikiheshimiwa  kama shirika la Kidini.  Na hatua zilizochukuliwa kuuunda muundo  wake mpya wa kisheria, hutangaza wazi kwamba, utendaji wa usharika huu, iwe ndani ya Kanisa au kwa ajili ya dunia, ni lazima kushiriki katika utume wa Kanisa. Kwa kuwa ni upendo katika ukweli, uliojikita katika asili ya  Upendo wa Mungu  na uzoefu wa Kanisa la Mwanzo,  kuuweka upendo katika mazingira yake ya awali, ya  kutangaza Neno la Mungu na maadhimisho ya sakramenti, kama kipaumbele cha kwanza  sahihi na muhimu kwa  Kanisa. Hivyo basi,  kabla ya kuigia katika utendaji  ngazi za jamii, ni lazima kuthibitisha kwamba hisani za Kanisa, zinakuwa na tabia ya Kikanisa.

Kanuni hiyo, inakuwa ni rejea msingi , katika uanzishaji wa  huduma zote za hisani za Kanisa Katoliki  na utendaji wake wote, unaelekezwa kwa Mungu, kwa kuhamasishwa upendo kwa jirani, kupia fadhila na utoaji wa msaada kwa kila binadamu, kama  Bwana alivyofundisha na kutenda .  Ni wazi, na ni muhimu kwa Wakristo , kutafakari na  kutafuta ufumbuzi wa pamoja kwa  matatizo mengi ya umaskini na kutengwa kama  sharti la haki. Lakini, wakati huohuo ni muhimu pia kufikiria uwepo wa mbinu zinazoweza fanikisha ufanisi wa huduma  hii ya kanisa, bila kuhatarisha au  kupoteza tabia yake ya  Kikristo  katika kazi zake. Zaidi ya yote,  jinsi kanisa linavyoweza kukabiliana na  mateso ya binadamu na umaskini, kupitia huduma  ya  huruma na wema unaofundishwa katika moyo wa ujumbe wa injili.

Hilo huhakikisha utimizaji wa wajibu msingi na  muhimu ndani ya Kanisa na jamii kwa ujumla. Hivyo isisahaulike kwamba,  Caritas ina utambulisho tofauti na  taasisi na vyama vingine vingi.  Katika Kanuni zake,   Caritas  katika ngazi ya jimbo,  ni chombo cha Askofu kwa ajili huduma katika utume wa upendo na mshikamano wa Askofu kwa watu wahitaji. Utambulisho huo ndiyo hasa hutofautisha  Caritas na taasisi au vyama vingine vinavyoweza anzishwa na  waamini Katoliki  Lengo la kwanza la Caritas  ni kuhamasisha watu juu ya upendo na utume wa Kanisa, ili watu waweze kuona upendo na huruma ya Mungu. N  Caritas inaweza kutoa mchango muhimu kufikia lengo hili, kama Papa Francis, alivyoomba, Caritas kuwa chombo Kikuu cha Kanisa Katoliki katika utoaji wa huduma za hisani za Kanisa,katika kuwaleta watu karibu zaidi na Mungu na ili Kanisa lenyewe liwe mlango wa upendo na wema.  








All the contents on this site are copyrighted ©.