Mapema Jumatatu hii katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, Kardinali Angelo Sodano , Mkuu wa Dekania ya Makardinali, aliongoza Ibada ya Misa katika Madhabahu Kuu ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, kwa nia ya kuadhimisha mwaka mmoja kupita tangu Mapapa Yohana XXIII na Yohana Paulo 11 walipotangazwa kuwa Watakatifu. Makardinali wengine walioshiriki katika Ibada hii ni Kardinali Angelo Comastri, Kardinali Leonardo Sandri na Kardinali Stanislaw Dziwisz, aliyekuwa amefuatana na ujumbe mkubwa kutoka Krakow Poland.
Kardinali Stanslaw Dziwisz , akihubiri katika Ibada hii, alimshukuru Kardinali Angelo Sodano , kwa huduma yake ya wakati alipokuwa Katibu wa Jimbo Takatifu kwa zaidi ya miaka kumi na minne alimotumikia kanisa kama mshirika wa karibu wa Papa Yohana Paul II, hadi ilipofariki Aprili 2, 2005. Kardinali Dziwizs , ameonyesha imani yake kwamba, Kardinali Sodano, bado anaendelea kuwa msaada mkubwa pia kwa Mahalifa wa Petro, na utume wa Kanisa,kwa ujumla. Na kwa namna ya kipekee kwa niaba ya Kanisa la Krakow na raia wa Poland, alitoa shukurani wale wote waliochangia kufanikisha maisha matakatifu kwa Yohana Paulo II, na hasa Papa Mstaafu Benedict XVI na Papa Francisco na pia Mkuu wa Shirika kwa ajili ya utajaji wenye Heri na Watakatifu Kardinali Angelo Amato.
Homilia ya Kardinali Dziwizs, iligeukia pia masomo ya siku , ikisema katika kumbukumbu hii ya kupita mwaka mmoja tangu watumishi hawa wa Mungu kutajwa Watakatifu, masomo yameongeza furaha na uelewa zaidi katika adhimisho hili , kwa kuwa yanayoonyesha kupitia jina la wavuvi wa Galilaya, Kristo alichagua na kujenga msingi wa Kanisa, alimosimika jumuiya kubwa ya wanafunzi wake, ambao leo wanaishi duniani kote. Kanisa lililoendelea kuchanua tokeo kaburi la Mtakatifu Petro, mfuasi wa kwanza wa Yesu Kristo, aliyemshuhudia Bwana wake , katika mji huu wa Roma, uliokuwa mji wa kipagani hadi kumwaga damu yake. Kardinali Dziwisz, alieleza na kutaja maneno ya Yesu kwa Petro , Tunza kondoo wangu, akisema , maneno hayo yalimpa Petro nguvu mpya ya kumtumikia Bwana wake.
Kardinali aliendelea kuyatazama mazingira ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro akisema, ndani mwa Kanisa hili mna makaburi ya waandamizi wengi wa Askofu wa kwanza wa Roma. Na miaka kumi iliyopita, kuliongezeka kaburi jingine la halifa wa Petro aliyelichunga Kanisa kwa karibia miaka ishirini na saba, Petro wa miaka yetu, tunayeyajua maisha yake, Yohana Paulo II, anayeitwa kabla Karol Wojtyla, ambaye wito wa kumtumikia Bwana wake ulioanzia Wadowice na baadaye Krakow, kupata ukomavu zaidi alipokabidhiwa kuliongoza Kanisa la Ulimwengu hapo Oktoba 16, 1978. Hivyo uzoefu wa Simon Petro ukawa uzoefu wake binafsi. Mahali hapa ambapo Simon Petro, alikuja kutoa ushahidi wake wa hali ya juu, ndivyo ilivyokuwa kwa halifa wake Yohana Paulo II, aliyetaka kuondolewa uhai kwa kupigwa risasi, kutokana na upendo wake kwa Kristo na jirani.. Yohana Paulo aliyejaliwa busara daima katika kuonyesha uzoefu wa maisha timilifu, daima alijiweka katika mikono ya Kristo, kwa imani kwamba Kristo alijua udhaifu wake wa kibinadamu. Na hivyo alimpa Kristo nafasi ya kwanza kuyaongoza maisha yake . Aidha Kardinali alikumbuka siku ambayo Yohana Paulo II alipotangazwa Mwenye Heri na Papa Benedikto XVI, miaka minne iliyopita, katika Jumapili ya Huruma ya Mungu, akirejea sauti za watu watu wa Mungu zilivyomlilia wakati wa kifo chake, atangazwe Mtakatifu mara moja "Santo subito". Tamko lililoonyesha hamu ya watu wa Mungu kwamba, jina lake lisibaki katika vitabu vya historia ya kanisa tu, lakini aendelee kuongozana wanafunzi wa Yesu, aliyesulubishwa na kufufuka, Bwana wa njia ya imani, matumaini na upendo katika dunia yetu yenye hofu na mashaka.
Kardinali Dziwizs anasema , utakatifu si upendeleo kwa wanafunzi wachache tu wa Yesu. Utakatifu ni wito kwa watu wote wa taifa la Mungu, kama ilivyosisitizwa na kuwekwa wazi nusu karne iliyopita na Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican. Utakatifu ni kwa wote wanaomwamini Kristo. Utakatifu haujali cheo au hadhi, lakini wote wameitwa kuishi maisha yenye utimilifu wa Kikristo yaani ukamilifu wa upendo" (Lumen Gentium, 40), wote wameitwa katika kuwa Watakatifu na Yohana Paulo 11, anakuwa ni mfano hai wa maisha matakatifu yenye kuwavutia watu kwa Mungu. Mtakatifu Yohana Paulo II , alikuwa ni mtu wa maombi, tafakari na mhudumu, aliyeyatolea maisha yake bila kujibakiza kwa ajili ya wengine. Alimpenda Yesu Kristo kwa upendo Mkuu , na katika upendo huu aliweza kutoa huduma bila kuchoka kwa Kanisa na kwa dunia. Yeye alifanya kila kitu kwa kila mtu, kwa ajili ya kuifikisha habari njema katika miisho yote ya dunia.
Kardinali alieleza na kumshukuru Mungu kwa zawadi hii ya Mtumishi wake Mtakatifu Yohana Paulo II, ambaye anaendelea kuliiimarisha Kanisa zima hata leo hii. Na hivyo sasa yeye ni mwombezi wetu mkubwa mbinguni; kwa sababu zetu binafsi, familia na jamii. Kardinali Dziwizs alieleza na kutoa wito kwa watu wote kwama, kumbukumbu hii ya wazi ya Papa Yohana Paulo II katika maisha matakatifu, idumu katika mawazo yetu na katika mioyo yetu, na maisha ya kanisa aliloluhudumia kwa njia tofauti. Na aambatanenasi katika njia yetu ya imani, matumaini na upendo.
Hata hivyo Kardinali pia akatahadharisha kwamba, hatuwezi kuishi tu katika kumbukumbu
hizi , lakini inakuwa ni changamoto iliyoko mbele yetu,yenye kugusa mioyo yetu na
Kanisa zima na taifa na hasa Kanisa nchini Poland. Ushahidi wa Yohana Paulo II, unapaswa
kushuhudiwa kwa ndugu zetu na dada zetu ambao bado hawajalijua kanisa , ambao bado
hawajajua kuwa Yesu ni Bwana na Mwokozi wao. Na aliwataka Waamini wajichotee urithi
wa ujasiri wa Yohana Paul II, na kutembea nao katika njia ya maisha ya upendo kwa
Mungu na jirani, yaani, kwa njia ya utakatifu. Hiyo ndiyo sala ya muumini kwa maisha
yake ya kila siku, sala anayopaswa kuitimiza.
Alikamilisha kwa kutolea maombi yake mbele ya Kaburi la Mtakatifu Petro, Mtakatifu Yohana XXIII na Yohana Paulo II, pamoja na Mama wa Kristo, mbele ya kiti cha Huruma ya Mungu, kwa ajili ya kujaliwa zawadi ya imani iliyo hai, tumaini thabiti na mapendo thabiti.
All the contents on this site are copyrighted ©. |