(Vatican Radio) Jumanne 7 April ilikuwa Siku ya Afya Duniani." Unatakiwa kujali kila unachokula kwa kuwa kinaingia mwilini mwako !“ Ni angalisho lililotolewa katika kuadhimisha siku ya Afya ya Dunia kwa mwaka huu, adhimisho la kila tarehe 7 Aprili kama ilivyoteuliwa na Umoja wa Mataifa . Mwaka huu adhimisho lililenga zaidi katika usalama wa chakula , tangu kinapozalishwa hadi kinapomfikia mlaji mezani. Shirika la Afya la Dunia "WHO",limetoa hoja hiyo kama kujali ongezeko kubwa na maradhi yanayotokana na chakula kibovu.
Shirika la Afya Duniani, linaitaja Siku hii 7 Aprili, kuwa fursa ya kuuelimisha
umma, changamoto na matatizo yanayohusiana na ukosefu wa chakula salama. Kaulimbiu
ya mwaka huu ikiwa "Kutoka shambani hadi katika sahani, fanya chakula salama”. Takwimu
mpya za madhara yanayosababishwa na magonjwa yanayo tokana na chakula zimekuwa ni
kitisho cha kimataifa, na hivyo kuzua haja ya kuwa na uratibu wa karibu katika mlolongo
mzima wa hatua zote zinazo hitajika tangu uzalishaji na usambazaji chakula hadi
kinywani kwa mlaji.
Dr Kazuaki Miyagishima, Mkurugenzi wa Shirika kwa ajili ya Usalama wa chakula katika
Idara ya Elimu ya Afya katika Umoja wa Mataifa, anasema usalama wa chakula ni tatizo
kubwa katika afya ya umma. Leo hii chakula si salama kutokana na kuchafuliwa na mambo
mengi kama virusi, bakteria, vimelea na kemikali, na kusababisha zaidi ya magonjwa
200 mbalimbali. Na hivyo Sekta mbalimbali zinazo husiana na shughuli zinazo gusa
chakula, kama vile kilimo, uvuvi, viwanda, utalii, biashara, vinapaswa kushirikiana
kwa ajili ya kuhakikisha chakula kinakuwa ni salama katika hatua zake zote hadi kinapofika
katika kinywa cha mlaji.
Pia ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu Dr Margaret Chan wa WHO, unasema, katika mazingira
ya utandawazi , hasa biashara huria iliyotengeneza fursa nyingi mpya hasa katika
usambazaji wa haraka wa chakula, imetoa pia mianya mingi ya kusambaa kwa haraka vimelea
na bakteria wa hatari na chakula kilichofuliwa na kemikali. Na hivyo sasa tatizo
la usalama wa chakula la mitaani kwa haraka linasambaa kwa haraka sana na kuwa dharura
ya kimataifa. Na kuzuka kwa ugonjwa unaotokana na chakula, linakuwa ni tatizo ngumu
kutatua kwa kuwa chakula kilichoko katika sahani moja au kutoka katika paketi moja
ya chakula kutoka nchi nyingine, inakuwa ni kazi kubwa kufuatilia asili ya chakula
kilipotoka.
Chakula kisicho salama hudhuru kwa uwepo wa bakteria, virusi, vimelea au kemikali
, ikisababisha aima mbalimbali za maradhi tangu kuharisha, hadi saratani. Mifano ya
vyakula visivyo salama ni kama vile vinavyoliwa bila kupikwa, vyakula vyenye asili
ya wanyama, matunda na mboga zilizolimwa katika mazingira machafu au kutoteshwa kwa
kutumia mbolea ya kinyesi, na pia samakigamba waliouawa kwa sumu na kuvuliwa baharini,
na watu wenye uchu wa fedha za harakaharaka .
Taarifa inaendelea kutoa mfano vijidudu aina ya Salmonella Typhi , husababisha
wastani wa vifo 52,000, wakati aina ya E. coli huua wastani wa watu 37, 000, na
norovirus huua watu 35,000 kwa mwaka. Na kwamba, idadi kubwa ya maradhi yanayotokana
na chakula na vifo hutokea Afrika ikifuatiwa na Kusini-Mashariki mwa Asia na zaidi
ya 40% ya watu wanaosumbuliwa na maradhi haya yanayosababishwa na chakula kichafu
ni watoto wenye umri chini ya miaka 5.
Hivyo WHO, linafanya jitihada za kidharura, kwa ajili ya kufanikisha njia za maendeleo chanya katika mifumo mikubwa ya usalama wa chakula, kwa kuhusisha serikali na hatua za umma katika kulinda chakula dhidi ya uchafuzi kemikali au vijidudu au virusi. WHO inachukua hatua madhubuti kitaifa na kimataifa, katika ufanikishaji wa jukumu muhimu hili muhimu katika kukuza usalama wa chakula tangu shambani hadi mezani,Ofisi ya habari ya WHO imeripoti.
imehaririwa na tjmhella -Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |