Kama ulivyo utamaduni wa Mapapa kwa Siku Kuu ya Pasaka , Papa Francisco majira ya adhuhuri , alitoa ujumbe wake kwa jiji la Roma na Dunia kwa ujumla , mbele ya umati mkubwa wa mahujaji na waamini waliofurika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro.
Alisema , Yesu Kristo amefufuka! Upendo umeshinda chuki, uzima umekishinda kifo
, mwanga umeipiga giza. Yesu kwa upendo wake kwetu, kwa hiari yake alivua utukufu
wake wa Kimungu , na, akatwaa namna ya mtumwa akajinyenyekeza hata kifo, mauti ya
msalaba. Kwa sababu hii Mungu amemtukuza na kumfanya Bwana wa ulimwengu. Yesu ni Bwana!
Ujumbe wa Baba Mtakatifu unawahakikisha binadamu wote kwamba , kwa kifo na ufufuo
wake, Yesu anaonyesha kwa kila binadamu njia ya maisha na furaha, na njia hii ni
kuwa mnyenyekevu na kukubali hadi kudhalilishwa. Maisha ya namna hiyo ndiyo huongoza
katika utukufu. Ameonya ni tu wale ambao ni wanyenyekevu wanaoweza kusonga mbele
katika njia hii inayoelekea juu kwa Mungu (cf. Wakosai 3: 1-4). “Wenye kiburi hutazama
chini kutoka juu na wanyenyekevu hutazama juu tokea chini."
Baba Mtakatifu ameeleza na kurejea somo la Asubuhi ya Pasaka, ambamo wanawake, waliwahimiza
Petro na Yohana kwenda mbio kutazama Kabuni, Nao walikuta li wazi na tupu. Walijongea
lango la kaburi, wakainamisha vichwa vyao ili waingie kaburini. Papa amesema , hiyo
ndiyo siri ya kuingia katika fumbo hili la wokovu , tunahitaji kuinamisha maisha yetu
katika unyenyekevu, kusikiliza Neno la Mungu na kuliishi kwa hiari. Ni kwa namna
hiyo tu, mtu anaweza kuelewa utukufu wa Yesu na kuwa na uwezo wa kumfuata katika
Njia yake.
Papa alibaini , dunia inasema , ili kusonga mbele katika maisha ni lazima, kupania
hivyo kwa gharama zote katika hali ya ushindani.. Lakini Wakristo wanaamini , kwa
neema ya Kristo, aliye kufa na kufufuka, ndiyo mbegu ya ubinadamu wote, unaotafutwa
na binadamu katika kuhudumiana , mmoja kwa mwingine, wala si katika kuwa kiburi,
lakini badala yake ni katika kuheshimiana na utayari wa kusaidiana.
Kuheshimu wengine haina maana ya kuwa dhaifu, lakini nguvu ya kweli! Wale ambao
kubeba yao Ndani ya nguvu za Mungu, upendo wake na haki yake, hawana haja ya kutumia
vurugu, bali wao ni watu wa kuzungumza na kutenda kwa nguvu ya ukweli, fadhila na
upendo.
Papa alieleza na kuomba kutoka kwa Bwana Mfufuka neema ya kutoanguka katika majaribu
ya majivuno na ufahali wenye kuchochea vurugu na vita, lakini katika kuwa na ujasiri
wa kusamehe kwa unyenyekevu na amani. Aliendelea kumwomba Yesu , Mshindi wa kifo,
kupunguza mateso ya ndugu zetu Wakristo wanaoteseka kwa Jina lake, na wale wote
ambao wanadhulumiwa kama inayojionyesha sasa katika migogoro na vurugu zinazoendelea
kusikika duniani kote. matokeo ya migogoro inayoendelea na vurugu.
Papa ameomba kwa ajili ya amani , na hasa kwa ajili mataifa yanayoteswa na vita na
fujo kama Syria na Iraq, ili kwamba sauti ya silaha iweze kunyamaza na ili mahusiano
ya amani, yarejeshwe miongoni mwa makundi mbalimbali yanayoishi katika mataifa hayo
pendwa . Na pia ameitaka jumuiya ya Kimataifa isijitenge mbali na majanga haya yaliyo
nje ya ubinadamu, yanayojitokeza katika nchi hizi na kusababisha watu kuishi katika
hali duni Ukimbizi.
Aidha Papa ameomba kwa ajili ya amani kwa watu wote katika Nchi Takatifu, ili waweze kukua katika utamaduni wa kukutana hasa kati ya Israel na Wapalestina , na ili majadiliano na mchakato wa ya kurejesha amani , na mchakato wa amani kuwa tena, ili kukomesha miaka ya mateso na mgawanyiko.
Na pia kwa ajili ya amani Libya, ambako kuna ujinga wa umwagaji damu na vitendo
vyote ushenzi na vurugu viweze kusitishwa, na kwamba wote waweze kuishi kwa amani
na mustakabali wa nchi, uweze kujengwa katika neema ya kufanya kazi kwa maridhiano
na ujenzi wa ya udugu na mshikamano wenye kuheshimu utu wa mtu. Na ndivyo iwe kwa
Yemen pia, ambapo wote wana hamu ya kuona ukuaji wa amani, kwa manufaa ya watu wote.
Papa aleleza na kuweka tumaini lake katika huruma ya Bwana kwamba makubaliano yaliyofikiwa
Lausanne, yaweze kuwa hatua mbele thabiti katika ujenzi wa usalama na udugu duniani.
Aidha Papa amehimiza maombi kwa Bwana Mfufuka kwa ajili ya zawadi ya amani kwa
mataifa kadhaa ya Afrika , yanayosumbuliwa na ghasia na fujo za umwagaji wa damu kama
ilivyo nchini Nigeria, Sudan Kusini na maeneo mbalimbali ya Sudan na Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Congo. Papa anaomba sala namaombi ya watu wenye mapenzi mema na ziweze kupekelewa
na Bwana kwa ajili ya wote waliopoteza maisha ya. Na kwa namna ya kipekee amewakumbuka
vijana waliouawa Alhamisi iliyopita katika Chuo Kikuu cha Garissa Kenya , na wote
waliotekwa nyara , au wale waliolazimishwa kuachana na makazi yao au wapendwa wao.
Papa pia hakuchelea kuomba mwanga wa Bwana Mfufuka , ulimulikie taifa la Ukraine, hasa kwa wale ambao wamevumilia vurugu na mgongano katika wa miezi ya karibuni. Ameliombea taifa hilo limeweze kugundua upya amani na matumaini kupitia uwajibikaji na dhamira ya vyama vyote.
Papa pia alitoa mwaliko wa kuombea amani na uhuru kwa ajili ya wanaume na wanawake
wengi , ambao sasa wameingizwa chini ya mfumo wa zamani na mpya ya utumwa na watu
binafsi au makundi ya uhalifu. Pia kwa ajili ya amani na uhuru wa waathirika wa
wafanyabiashara wa madawa ya kulevya, ambao mara nyingi wana ubia na mamlaka yanayotakiwa
kulinda amani na maelewano katika familia ya binadamu. Pia ni kuomba amani kwa dunia
hii inayokabiliwa na wafanyabiashara wa silaha.
Mwisho Papa ,aliwakumbuka wote wanaohangaika kimaisha , akianza na wale waliotelekezwa
pembezoni na jamii, waliofungwa jela, maskini na wahamiaji ambao ni hivyo mara nyingi
hupambana na kukataliwa, wenye kudhulumiwa , wagonjwa na mateso mengine, watoto, hasa
waathirika wa unyanyasaji, ambao leo hii wamegubikwa katika huzuni na maombolezo,
na wote na wanawake kwa waume wenye mapenzi mema , waweze kusikia na kufarijiwa
na sauti ya Bwana Yesu akisema : "Amani kwenu" (Lk 0:36). "Msiogope, kwa maana Nimefufuka
na daima nitakuwa Nanyi.
Baada ya kusoma ujumbe wake , Papa alisalimia kwa kutaja makundi mbalimbali ya
mahujaji waliofika katika uwanja huu wa Mtakatifu Petro, tokea pande mbalimbali za
dunia, na kwa wote walio kuwa wakimsikiliza kupitia njia za mawasiliano jamii. Kwao
wote aliwapa Baraka zake za Kipapa za Pasaka , akiwatakia kila lililo jema katika
nyumba zao na wote wanaoishi nao au kukutana na katika kuitangaza furaha la Maisha
Bwana Mfufuka , aliyeleta pamoja naye upendo, haki, heshima na msamaha.
alikamilisha na asante kwa uwepo wao, kwa ajili ya maombi yao na shauku yao katika
imani yako.
Na pia alitoa shukurani kwa Taasisi ya Uholanzi iliyopamba uwanja wa Kanisa Kuu la
Mtakatifu kwa ajili ya Siku Kuu ya Pasaka.
All the contents on this site are copyrighted ©. |