2015-04-01 16:09:00

Papa-Maadhimisho ya Pasaka ni kuliishi fumbo la Pasaka


Kama kawaida ya kila Jumatano, majira ya asubuhi, Baba Mtakatifu  alitoa katekesi  yake kwa mahujaji  na wageni waliokusanyika katika  Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro . Katika katekesi hii alianza kwa kuitaja  Alhamisi Kuu ambamo ,kwa Ibada ya Karamu ya Mwisho ya Bwana ,  hukifungua kipindi cha Siku Tatu Kuu tatu kuelekea adhimisho la Fumbo la Pasaka, “Triduo Pasquale “ ambamo mna mateso, kifo na ufufuko wa Bwana, ikiwa ni kilele cha mwaka mzima wa Liturujia na pia hatima ya maisha yetu ya Kikristo.

Alisema , Siku Kuu hizi Tatu , huzinduliwa na maadhimisho ya karamu ya mwisho ya Bwana. Yesu katika usiku wa mateso yake, aliutoa mwili wake kwa Baba, mwili wake na damu yake kupitia alama za chakula , Mkate na mvinyo , akiwalisha Mitume wake na kuwataka waendeleze  hili kwa ukumbusho wake.  Papa ameendelea kuzungumzia Injili  inayosomwa katika tukio hili la Alhamisi Kuu, akikumbuka jinsi Yesu alivyoosha miguu wanafunzi wake, ishara ya huduma, fadhila na unyenyekevu. Na alitaja pia maana ya tukio hilo katika mtazamo wa Yesu katika  Ekaristi.. Alifafanua , Yesu anawaosha miguu mitume wake kama  mtumishi. Aliiosha miguu ya Petro na wanafunzi wake wengine kumi na moja wanafunzi (cf. Jn 13.4-5). Kwa ishara hii ya kinabii, anaonyesha hisia ya maisha yake na mateso yake, kwamba ni huduma kwa Mungu na kwa wengine:akiyatimiza maneno yake mwenyewe, "Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumika" (Marko 10:45).
 

Hii pia inaonyesha kilichotokea katika ubatizo wetu, wakati neema ya Mungu, inatutakasa dhambi na sisi kujiweka  kwa Kristo (Kol 3:10).  Na ndivyo inavyotokea  kila wakati waamini wanapofanya kumbukumbu ya Bwana katika Ekaristi: inakuwa ushariki na Kristo Mtumishi,  kwa kutii  amri yake ya upendo, kupendana kama Yeye alivyotupenda (cf. Jn 13:34; 15:12). Lakini Papa ameonya katika umoja huu  Mtakatifu, ni lazima kuwa na utambuzi wa dhati, katika utayari wa kuhudumiana  mmoja kwa mwingine ili tuweze  kuutambua  Mwili wa Bwana.  Yesu aliutoa sadaka mwili wake kikamilifu katika huduma. 

Kisha Papa alizungumzia pia Liturujia ya Ijumaa Kuu ambamo waamini wanatafakari Fumbo la mateso na Kifo cha Kristo na kuabudu Msalaba . Amesema kwa kuyatoa maisha yake sadaka msalabani , dhambi zetu zote zinaondolewa kupitia upendo wake , upendo kamili tunaotakiwa kuuishi na kuueneza.. Katika dakika za mwisho za maisha yake , kabla ya kukabidhi  roho kwa  Baba, Yesu alisema: yametimia (Yohana 19:30). Papa amefafanua zaidi kwamba, Neno hili imetimia lina maana kwamba Yesu, kazi ya wokovu imetimia, kwamba maandiko yanatimilika katika upendo wa Kristo, Mwana kondoo anayeuawa. Yesu, kwa sadaka yake ya maisha , alifanya mageuzi katika  ukosefu wa usawa,  kwa upendo  mkuu.. Upendo huu umekuwa ukishuhudiwa kwa karne na karne na wanaume na wanawake, kwa  ushuhuda wa maisha yao, yenye kutoa  miali ya tafakari juu ya upendo kamili, upendo kamili usiokuwa na doa. 

 

Papa alieleza hilo na kutoa mfano wa ushahidi wa kishujaa wa wakati wetu, wa  Padre  Andrea Santoro, Padre wa  Jimbo la Roma na Mmisionari ,aliyeuwa  Uturuki, ambaye siku chache kabla kuuawa huko  Trabzon, aliandika hivi: "Mimi naishi hapa kati ya watu hawa, nikimruhusu Yesu  afanye hivyo kupitia kwangu . Yesu aliweza  tu kuleta wokovu, kwa kutoa mwili  wake  mwenyewe sadaka, Na ndivyo ili  kuyashinda. maovu ya dunia, ni  lazima machafu na maumivu yote kwa  pamoja, yamwilishwe katika nyama yao wenyewe njia, kama Yesu alivyofanya "

 

Papa aliomba mfano wa imani ya mtu huyu wa nyakati zetu, na wengine wengi, viweze kutusaidia katika kutoa sadaka ya  maisha yetu kama zawadi ya upendo kwa ndugu, tukimwiga  Yesu Mwenyewe

Papa alikamilisha mafundisho yake na tafakari juu ya  Jumamosi Kuu  ambamo kwanza tunauona mwili wa Yesu ukiwa umelala kaburini , wakati wa giza nene la  usiku, linaloonekana wakati  mwingine kutaka kupenya katika nafsi zetu ,na kukatisha tamaa nguvu ya upendo, ikififishwa na giza.  Lakini  giza hili,  linashindwa taa na moto wa  upendo wa Kristo, wenye kugeuza  mawe ya maumivu na mateso , na kuwa  nafasi ya matumaini. Hapa ndipo kuna  siri kubwa ya Pasaka!

Katika usiku huu Mtakatifu, Kanisa linapata kumulikiwa na mwanga wa Mfufuka. Na likiwa  Maria, Kanisa linakesha macho kwa mwanga wa imani,  na katika kila tumaini.  Papa  alieleza na kusisitiza kwamba , katika siku hizi tatu si tu kufanya maadhimisho ya kumbukumbu lakini ni wakati wa kuzamisha mioyo yetu ndani ya fumbo hili la wokovu , tukikiishi  kipindi hiki na hisia za kweli za uwepo wa  Kristo ndani mwetu.  Kwa namna hiyo ndivyo tunaweza kupokea baraka za Pasaka.

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.