2015-03-25 14:28:00

Juhudi za Umoja wa Mataifa katika malengo ya milenia


Kwa ajili ya maandalizi ya Mkutano muhimu wa Kimataifa utakaofanyika Addis Ababa , mwezi Julai 2015,  juu ya utekelezaji wa  malengo  endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs) , watalaam wa uchumi kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa , hivi karibuni walikutana mjini Geneva ,mazungumzo yaliyo fadhiliwa na Tume ya Uchumi kwa Ulaya . Mkutano huo ulijadili utekelezaji wa  malengo ya maendeleo kama changamoto kubwa katika upatikanaji wa  matrilioni ya dola kwa kila  mwaka.


Amina Mohammed, Msaidizi wa  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,ambaye pia ni Mwakilishi Maalum katika Mipango ya Maendeleo ya baada ya Malengo ya mwaka 2015, alizungumza katika mkutano huo, kwa kutoa wito kwa mataifa kwamba,  umefika wakati kwa serikali kuwajibika zaidi na hatua za  utekelezaji kwa  ahadi walizotoa.

 

Mwandishi wa habari hii Daniel Johnson, anaendelea kumnukuu Bibi Amina Mohammed, kwamba kwa  hitaji la kiwango cha trilioni kati ya $ 5 hadi wa $ 7 kwa mwaka, kwa ajili ya miradi ya miundombinu peke yake ni muhimu kuwa na mikakati tangu sasa, katika  jinsi ya kupata fedha hizo.  Na kwamba , changamoto kama vile kutokomeza umaskini ifikapo mwaka 2030 na kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa, yana mwelekeo wa kugharimu  fedha nyingi  zaidi  na hasa iwapo mataifa hayatajipanga vyema,  katika kutimiza ahadi zake za kifedha.

Amina Mohammed, aliendelea kusema kwamba kuna kila aina ya majawabu  yaliyowasilisha mezani  kimsingi yakionyesha mazingira ya uwepo wa nyenzo za kupata fedha, tena  si tu mabilioni, lakini matrilioni ya fedha zinazohitajika. Lakini fedha hizo zitapatikana iwapo serikali zitawajibika katika kushika usukani wa kufanikisha  malengo 17 ya Umoja wa Mataifa, yanayo waniwa na  wote.  Bi Mohammed  kati ya changamoto nyingi zilizowasilishwa mezani, ametaja haja ya kukomesha  ukwepaji wa kodi na mtiririko wa fedha haramu.

Aidha alitaja utayari wa sekta binafsi kushirikiana katika utafuta wa matrilioni ya dola zinazo hitajika, lakini sekta hiyo imefungwa na baadhi ya vipengere vinavyo hitaji kulegezwa.

 Matokeo ya mkutano Geneva yatatumika katika mkutano muhimu wa kutafuta ufadhili katika mipango ya maendeleo, utakao fanyika  Addis Ababa mwezi Julai 2015.








All the contents on this site are copyrighted ©.