2015-02-26 15:17:40

Vita, fujo na ghasia vilipamba moto sana mwaka 2014


Mwaka 2014 unaweza kupewa sifa za kuwa mwaka wa ghasia za mapigano na fujo, zilizo sababisha majanga kwa mamilioni ya watu walionaswa katikati ya ghasia hizo. Ripoti ya mwaka ya Asasi ya Kujitegemea “ Amnesty International”, imeeleza baada ya kuchambua hali ya utulivu na amani katika nchi 160 na kusema ni aibu utendaji wa kimataifa, kushindwa kukabiliana na ghasia hizo na mauaji yanayo fanywa na makundi ya waasi.

Rais wa Amnesty Italia, Antonio Marchesi , katika mahojiano na Francesca Sabatinelli, ameitaja ripoti hiyo kuwa ni hali halisi, inayozungumzia ukweli wa moja kwa moja kwa maisha ya mamilioni ya watu walio naswa katika migogoro yenye vurugu kuanzia Gaza, Nigeria, Syria, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Iraq, na mbele ya uso wa janga hili, jumuiya ya kimataifa imebaki mbali. Mwaka huu umeongoza kwa dunai kushuhudia machafuko mengi tokea miaka 70 iliyopita baada ya kuundwa kwa Umoja wa Mataifa. Dunia imeshuhudia vurugu nyingi katika ngazi ya kimataifa zenye kusababisha wimbi kubwa na wakimbizi na wahamiaji.
Antonio Marchesim, ameeleza kwa kurejea taarifa mbalimbali za mwaka 2014, zinazoonyesha idadi kubwa sana ya mauaji yaliyofanywa na serikali na makundi ya waasi, kwa njia vita, mfano mashariki mwa Ukraine, yaliyo rejesha Ulaya kuishi katika mazingira ya Vita Baridi. Ongezeko la nguvu za makundi binafsi kama yale yanayodai kupigania haki ya nchi kutawala kwa mtindo wa sheria za Kiislamu, kama vile Boko Haram na Al Shabaab.

Rais wa Amnesty Italia anasema, “Jumuiya ya kimataifa huwezi kujenga kuta, katika kulinda mipaka yake kwa mataifa kadhaa. Kuna dharura ya kibinadamu na nchi tajiri zinao wajibu wa kuingilia kati mgogoro wa kiuchumi, na nchi za kawaida na maskini pia lazima zifanye sehemu yake. Ameeleza kwa kutoa mfano kwamba, watu wengi wamekimbia kutoka Syria na kuingia Lebanon, Jordan, Uturuki, katika baadhi ya kesi nchini Iraq, si katika nchi za Ulaya. Wimbi hilo la wakimbizi haliwezi kuitwa wimbi la uvamizi, maana watu hao wanakimbia madhulumu halisi dhidi ya maisha yao.

Takwimu za mahusiano katika nchi 18 zimeonyesha kwamba, kumekuwa na uhalifu wa kivita au ukiukwaji mwingine wa "sheria za vita". Na katika nchi 35 kumekuwa na makundi ya waasi ya ukiukwaji wa haki na amani nakusababisha wakimbizi zaidi ya 3,400 na wahamiaji kufa maji katika bahari ya Mediterranean. Na wakimbizi 4 kutoka Syria –asilimia 95% , wanaishi katika nchi jirani na katika nchi 119, kumekuwa na vikwazo katika uhuru wa kujieleza. Amnesty International inataka si kupitisha mbinu kibabe na kandamizi katika kukabiliana na unyanyasaji na madhulumu kwa sababu jibu la nchi katika kukabiliana na vitisho hivyo , halipaswi kuhatarisha haki za msingi za binadamu. Na kwa kuwa utumiaji wa mabavu hauwezi kuwa suluhu ya kudumu katika migogoro mingi, anasema Marchesi.

Na hivyo, Amnesty International, imetoa wito kwa Wajumbe watano wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, kutoa mapema jibu lao kwa ujumla, kupitia njia rasmi ya nguvu yao ya Veto, wakati wanapojadili hali halisi za vurugu na mauaji ya kiholela au mauaji ya kimbari, ikiwemo adhabu zinazo stahili kwa makosa hayo. Hatua nyingine ni kuridhiwa kwa mkataba wa biashara ya silaha, ambayo imeridhiwa na nchi nyingi, lakini mataifa makubwa Marekani, Urusi, Canada, Israel, hawajaridhia mkataba huo. Ni jambo muhimu kwa mataifa makubwa kuridhia mkataba huu kama hatua muhimu katika kukomesha mzunguko wa silaha zenye kutumia kemikali za hatari” arsenals”, ambazo huishia katika mikono ya watu na hivyo kuleta wasiwasi mkubwa, wa kuangamiza maisha ya watu wengi wasiokuwa na hatia.








All the contents on this site are copyrighted ©.