2015-02-25 14:03:55

Tuzo ya Heshima ya Amani yamwangukia Esther Ibaga wa Nigeria


Tuzo ya Amani ya Heshima ya 32 ya Niwano, imemwangukia Esther Abimiku Ibanga, Mchungaji na mwanaharakati wa haki za wanawake nchini Nigeria, kwa kuchaguliwa kuwa mshindi wa tuzo ya amani ya Niwano ya 32.

Jopo la uteuzi la kimataifa na Shirika la Niwano Peace Foundation, limemteua Esther Ibanga , kwa kuridhika naye kwamba , si tu anatetea usalama wa maisha ya maelfu ya watu, lakini pia alianzisha shirika lenye kugusa maelfu ya wengine." Esther Abimiku Ibanga, Machi ya 2010 alianzisha Asasi inayo julikana kwa jina "Wanawake Bila Kuta" (Wowwi), kwa hamu ya kutaka kukomesha vurugu na mauaji kwa wanawake na watoto, katika Jimbo la Nyanda za juu nchini Nigeria.

Asasi hiyo ya kujitegemea, viongozi wake wametoka makundi yote ya kikabila Nigeria, na kama ilivyo asili yake, limekuwa ni muungano wa nguvu wa vikundi vya wanawake , dhidi ya mgawanyiko wa kikabila na kidini, muungano wa viongozi wanawake wakiwemo Wakristo na Waislamu. Jukumu lake ni kuonyesha jinsi wanawake wanavyo paswa kuwajibika katika kujenga amani.

Habari inafafanua kwamba, madhumuni ya juhudi hizi, ni kukuza mbinu shirikishi na njia bunifu zinazoweza kuwaunganisha Wanigeria bila vurugu katika kutatua migogoro ya kijamii na katika kufanikisha mageuzi Nigeria kupitia wanawake. Na pia miongoni mwa mambo mengine, ni kuunda muungano wa nguvu wa vikundi vya wanawake katika ngazi ya kitaifa na kimataifa, dhidi ya aina yoyote ya mgawanyiko, pia kutoa ufahamu juu ya umuhimu wa jukumu la wanawake katika kujenga amani. Juhudi hizi zimeutazama ukweli kwamba, katika migogoro mingi ya Afrika, ikiwa ni pamoja na Nigeria, wanawake na watoto huteseka kwa matokeo mabaya. Wakati huo huo, kama mama, wanawake ni waelimishaji wa kwanza wa wanadamu. Katika hali hii, kazi ya Ibanga inalenga kukuza na kutumia fursa za wanawake kama wapatanishi, na kutambua kwamba wanawake wanaweza kuwa na ushawishi nguvu katika maisha ya watu (baba, ndugu, waume na wana).

Shirika hili la Ibanga linakemea vikali utendaji wa kikundi cha Boko Haram. Na ili kuweka kufanikisha maono na malengo yake katiak juhudi za Wanawake bila Kuta, chini ya uongozi wa Mchungaji Ibanga, limechukua hatua za kuongeza nafasi za wanawake kwa njia upatikanaji wa ujuzi na misaada midogomidogo ya fedha. Mara kwa mara limekuwa likiandaa maandamano na bila kuchoka kutoa wito kwa viongozi wa serikali na wanasiasa, wajishughulishe zaidi na suala la dhuluma na unyanyasaji kwa wanawake, likipaza zaidi sauti ya akina mama na sauti chanya ya viongozi wa kidini dhidi ya wababe wa vita ambao wanatumia dini kuhamasisha vijana kufanya vurugu ili kukidhi nia ya ubinafsi wao.
Juhudi hizi dhidi ya ugaidi na ujenzi wa amani, "Wanawake Bila Kuta” mara ya kwanza, huandaa mazungumzo ya jamii na polisi, kwa nia ya kukuza uaminifu kati ya jamii na polisi katika jitihada za kukabiliana na ugaidi. Pamoja na mashirika mengine pia kukuzwa amani na mshikamano mashuleni, hasa katika mkoa wa Nyanda za Juu Nigeria, ambao umesongwa na madhulumu ya Boko Haram. Asasi hiyo pia huwakilisha wanawake katika mikutano ya kimataifa na vikao katika nchi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Rwanda, Afrika Kusini, Austria na Marekani. mchungaji Ibanga pia alikuwa mmoja wa wawakilishi wa wanawake katika mikutano ya Umoja wa Mataifa, uliozungumzia haja ya "kuzuia na kukabiliana na unyanyasaji na mauaji ya jinai dhidi ya makundi ya wachache".







All the contents on this site are copyrighted ©.