2015-02-12 15:17:02

Monsinyo Fernando Chica Arellano ateuliwa kuwa Mwakilishi wa Vatican: FAO, IFAD na WFP.


Baba Mtakatifu Francisko amemteua Monsinyo Fernando Chica Arellano kuwa Mwakilishi wa kudumu wa Vatican kwenye: Shirika la Kilimo na Chakula la Umoja wa Mataifa, FAO, Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo wa Umoja wa Mataifa, IFAD pamoja na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP. Kabla ya uteuzi huu alikuwa ni Mshauri wa Ubalozi wa Vatican.

Monsinyo Fernando Chica Arellano, alizaliwa kunako tarehe 24 Juni 1963. Baada ya masomo na majiundo yake ya kikasisi, akapadrishwa kunako tarehe 19 Aprili 1987. Baada ya kujiendeleza na kupata shahada uzamifu katika Mafundisho tanzu ya Kanisa, alianza huduma ya kidiplomasia mjini Vatican kunako tarehe Mosi, Julai 2002.

Tangu wakati huo ametekeleza utume wake kwenye Ubalozi wa Vatican nchini Colombia, Ubalozi wa Vatican kwenye Umoja wa Mataifa na huduma kwenye Sekretarieti ya Vatican kuhusiana na masuala ya jumla.

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.