2015-02-12 08:38:53

Cheche za matumaini na amani!


Mameya kutoka Nchi Takatifu baada ya kuhudhuria Katekesi ya Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 11 Februari 2015, wamekutana pia na kuzungumza na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican, wakionesha matumaini yao katika kukoleza mchakato wa matumaini na amani katika Nchi Takatifu.

Viongozi hawa wamemshirikisha Baba Mtakatifu: matatizo, changamoto na matumaini yao kwa Nchi Takatifu pamoja na kulishukuru Kanisa kwa huduma ya upendo na mshikamano unaooneshwa kwa wananchi huko Nchi Takatifu hasa katika sekta ya elimu, afya na huduma kwa jamii. Hospitali ya Watoto iliyoko Bethlehemu inahudumiwa na Kanisa kwa njia ya fedha ya wafadhili kutoka sehemu mbali mbali za dunia na kwamba, hii pia ni fursa ya ajira kwa wafanyakazi 238.

Hospitali ya Watoto ya Caritas Bethlehemu, ina uwezo wa kulaza watoto 82 na kila mwaka watoto wanaolaza Hospitalini hapo ni zaidi ya 4,000. Huu ndio utandawazi wa upendo, mshikamano na udugu; utandawazi unaoguswa na mahangaiko ya jirani.

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.