Baba Mtakatifu Francisko katika mahubiri yake kwenye Kikanisa cha Mtakatifu Martha
kilichoko mjini Vatican, Siku ya Jumanne, tarehe 10 Februari 2015, Kumbu kumbu ya
Mtakatifu Scholastica, mtawa na Bikira, amewataka waamini kufanya hija ya maisha ya
kiroho, ili kuutafuta uso wa Mungu, ili hatimaye, waweze kuwashirikisha wengine.
Wakristo
wasiojishughulisha katika maisha yao, kamwe, hawataweza kuufahamu uso wa Mungu na
hivyo kushindwa kumfahamu kwa ukamilifu zaidi. Hii ni hamu ambayo Mwenyezi Mungu amemwekea
mwanadamu katika sakafu ya moyo wake, inayomchangamsha kumtafuta Mungu, ili aweze
kuwashirikisha pia jirani zake. Utambulisho wa Mkristo unajionesha katika bidii ya
kutafuta kutekeleza mapenzi ya Mungu kwa njia ya mapendo na utimilifu wa Amri zake.
Kamwe mapokeo ya watu kisiwe ni kikwazo cha kutekeleza mapenzi ya Mungu, kwani
mwanadamu ameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu.
Na Padre Richard A. Mjigwa,
C.PP.S. Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.