Watumiaji wa teknolojia ya interneti nchini wametakiwa kutumia teknolojia hii kutafuta
taarifa mbalimbali za maarifa na zenye mwelekeo wa kuleta maendeleo badala ya kutumia
teknolojia hii kutafuta taarifa zisizo na faida na zenye mwelekeo wa kupotosha kizazi
cha sasa kimaadili.
Wito huu umetolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na
uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia, katika siku ya matumizi ya interneti
duniani iliyoadhimishwa leo duniani kote ambako alisema kuwa Vodacom kama kampuni
ya mawasiliano siku zote itakuwa mstari wa mbele kuwaelimisha wananchi juu ya matumizi
bora na sahihi ya mtandao wa interneti.
“Tukiwa kampuni inayoongoza kutoa huduma
za mawasiliano nchini siku zote tutashirikiana na serikali na wadau wengine wa masuala
ya mawasiliano kuhimiza matumizi bora na sahihi yamtandao wa internet.Matumizi ya
intaneti yamekuwa siyo anasa tena kama ilivyokuwa ikichukuliwa na wengi hapo awali
ambapo watu hujiunga kwa ajili ya kuwasiliana na watu walio nje ya nchi au kwa burudani
nyinginezo. Hivi sasa utumiaji wa intaneti umekuwa kutoka watu kuwasiliaina mpaka
kwa matumizi ya biashara ambapo watu wa mataifa mbali mbali hukutana mtandaoni kuuza
ama kununua bidhaa na huduma,”.Alisema.
Mbali na biashara alisema kuwa interneti
imejaa maarifa ya kielimu ya taaluma mbalimbali ambazo zinafanya dunia kuwa kijiji
kimoja hivyo matumizi mazuri ya interneti yanaweza kumfanya mtu popote alipo kupata
taarifa na maarifa ya fani anayohitaji au taarifa anazotaka kujua kwa haraka na kwenda
na wakati na kuna vyuo vingi duniani vinatoa elimu kwa njia ya mtandao. “Inashangaza
kuona baadhi ya watu hususani katika nchi zetu zinazoendelea wanatumia muda wao mwingi
kuangalia taarifa zisizo na manufaa kwenye mitandao ya interneti”.Alisema.
Aliwaasa
vijana wanaojiita wa kizazi cha Dot.Com hususani wanafunzi ambao wako mashuleni na
vyuoni kuachana na kutumia muda wao kutafuta taarifa za kuwapotosha na zisizoendana
na utamaduni wa kitanzania badala yake watumie teknolojia hii kupata maarifa na taarifa
zenye manufaa kwao na kwa maisha yao ya baadaye.
Alimalizia kwa kuwahimiza
watanzania kujiunga na mtandao wa Vodacom ambao hivi sasa unatoa huduma ya interneti
yenye kasi kubwa na viwango vya gharama nafuu lengo kubwa likiwa ni kuhakikisha idadi
ya watumiaji wa interneti nchini inaongezeka ili kwenda na nchi zilizopo katika ukanda
wa Afrika Mashariki.
“Katika kuhakikisha lengo hii linatimia hivi karibuni
tuliingiza kwenye soko simu za smartphone za gharama nafuu ambazo zimewalenga watu
wenye vipato vya chini hususani wanaoishi maeneo ya vijijini na tuna imani watazipenda
na kuzifurahia kwa kuwa mbali na kuwapatia interneti kwa gharama nafuu wakizinunua
wanakuwa wameunganishwa na mitandao maarufu duniani kama vile Facebook, Whatsap, Twitter,
Viber, Instagram na mingineyo”.Alisema.