Kanali Graf, mkuu mpya wa Vikosi vya Ulinzi mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko amemteua Luteni Kanali Christopher Graf, kuwa mkuu wa vikosi
vya ulinzi na usalama vya walinzi kutoka Uswiss, al maarufu kama Swissguars na kumpandisha
hadhi ya kuwa Kanali. Taarifa zinaonesha kwamba, uteuzi huu unaanza rasmi tarehe 8
Februari 2015.
Kanali Graf, alianza huduma ya ulinzi na usalama mjini Vatican
kunako mwaka 1987 na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Kanali Daniel Rudolf aliyeanza
kufanya kazi mjini Vatican kunako mwaka 2008 na mkataba wake kumalizika rasmi tarehe
31 Januari 2015
Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S. Idhaa ya Kiswahili ya
Radio Vatican.