2015-02-05 14:36:16

Athari za mabadiliko ya tabianchi!


Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi, tarehe 5 Februari 2015 amekutana na kuzungumza na Rais Anote Tong wa Jamhuri ya Watu wa Kiribati; baadaye amekutana na Kardinali Pietro Parolin, aliyekuwa ameandamana na Askofu mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.

Mazungumzo kati ya viongozi hawa wawili yamejikita katika umuhimu wa kulinda na kutunza mazingira pamoja na masuala mbali mbali yanayogusa mabadiliko ya tabianchi na athari zake nchini humo, kama ilivyo pia kwa nchi ambazo ziko kwenye Bahari ya Pacific, ambazo mwara kwa mara zinakabiliwa na majanga asilia. Mazungumzo haya yamelenga pia katika mkutano wa kimataifa utakaojadili kuhusu mabadiliko ya tabia nchi utakaofanyika mjini Paris, Ufaransa, Desemba 2015. Ni matumaini ya viongozi hawa wawili kwamba, Jumuiya ya Kimataifa itafanya maamuzi mazito na yanayotekelezeka ili kukabiliana na changamoto za athari za mabadiliko ya tabianchi.

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.