Askofu mkuu Thomas Luke Msusa ateuliwa kuwa Rais wa ECM
Taarifa kutoka katika mkutano wa Baraza la Maaskofu Katoliki Malawi inasema kwamba,
Maaskofu wamemchagua Askofu mkuu Thomas Luke Msusa kuwa Rais wa Baraza la Maaskofu
Katoliki Malawi. Itakumbukwa kwamba, Askofu mkuu Msusa pia ni mwanachama wa Kamati
kuu ya Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Afrika na Madagascar, SECAM.
Baraza
la Maaskofu Katoliki Malawi, limewachagua pia Maaskofu watakaosimamia shughuli mbali
mbali za maisha na utume wa Kanisa nchini Malawi, sanjari na kuwateuwa Maaskofu wawili
watakaowakilisha Familia ya Mungu nchini Malawi katika maadhimisho ya Sinodi ya Maaskofu
kwa ajili ya familia, yatakayofanyika mjini Vatican, Mwezi Oktoba, 2015.