2015-01-31 15:31:23

Mh. Sergio Mattarella, Rais Mpya wa Italia!


Baba Mtakatifu Francisko, Jumamosi tarehe 31 Januari 2015 amemtumia salam za pongezi Mheshimiwa Sergio Mattarella kwa kuchaguliwa kwake kuwa Rais Mpya wa Italia. Ni matumaini ya Baba Mtakatifu kwamba, Rais Mattarella atatekeleza dhamana na utume wake kwa ajili ya kujenga na kudumisha umoja wa kitaifa, amani na maridhiano nchini Italia.

Baba Mtakatifu anamwombea Rais Mattarella neema na baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu, ili aweze kumwangazia katika kazi yake, kwa ajili ya mafao ya wengi kwa kuzingatia tunu msingi za kiutu na maisha ya kiroho miongoni mwa wananchi wa Italia. Baba Mtakatifu anapenda kumpatia baraka kwake binafsi na kwa taifa zima la Italia.

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.