2015-01-26 14:31:08

I wapi haki, kunyamazisha sauti ya kidini katika huduma za afya ?


Bila sauti ya waamini kusikilizwa katika huduma za afya nani atatetea haki ya wanyonge? Ni maoni ya Daktari Denis Hunnell, Mtalaam katika huduma za Afya, aliyoyaandika katika makala yake ya tarehe 23 Januari na kunukuliwa ns shirika la habari za Zenit. Makala yanaonya dhidi ya unyamazishaji wa sauti ya kidini katika huduma za afya , kwa maelezo kwamba, bila imani kutumika katika uwanja wa huduma za afya, hapatakuwa na utetezi wa huduma za Afya hasa kwa makundi ya watu wanyonge katikajamii, kama wachanga, wazee na wagonjwa mahututi.

Dr Hunnel, amesisitiza kwamba, uhuru wa kidini, hutoa fursa ya utendaji katika misingi ya imani ya mtu katika kila nyanja ya maisha. Na kwamba Uhuru dhamiri zi zaidi ya muumini kuwa na uhuru wa kuhudhuria ibada, anayopenda. Lakini huwa ni maisha ya kweli katika chaguzi za utendaji wa maisha, kwa mujbu wa imani yake yenye kumuunganisha na maisha, familia, kitaaluma na kijamii, huku akishiriki katika mazoea yake ya kiroho, akiongozwa na matakwa ya imani yake, na misingi ya kuheshimu uhuru imani za wengine

Kwa bahati mbaya, ameonya daktari Hunell, “ tamaduni na desturi hizi msingi, zinazidi kusongwa na tabia za kukosa uvumilivu katika uhuru wa imani, kama ilivyo, kwa Wakristo wa Mashariki ya Kati na katika sehemu nyingi za Afrika, waamini wanateswa na kuchinjwa na Waislamu wenye msimamo mkali. Na katika ulimwengu wa Magharibi, tamaduni za kidunia, ingawa hakuna vurugu na kuchinjwa hadharani, kuna shinikizo la kutaka kutokomeza haki za imani za kidini katika maisha yote ya umma, kwa kuwa na sheria mbalimbali zinazogandamiza uhuru wa dhamiri, kama ilivyo huko Uingereza mfanyakazi alifukuzwa kwa kukataa kukiuka maadili yake ya kidini, kufungisha ndoa watu wenye jinsia moja.

Dr Hunell anaonya kuwa karibu katika kila taaluma, kuna hatari nyingi za dhamiri i kugandamizwa au kubaguliwa, na hasa katika taaluma ya utabibu. Wahudumu wa afya, wengi hulazimshwa kushiriki katika utendaji ulio kinyume na maadili yao ya kidini, mfano hushurutishwa kushiriki katika utendaji wa utamaduni wa kifo mfano utoaji wa mimba na eutanasia.

Wafanyakazi Katoliki, wanao wajibu wa kuzingatia Mafundisho Katoliki, yanayokiri maisha yote ya binadamu, yana hadhi kubwa, tangu wakati mimba inapotungwa hadi wakati wa w kifo cha kawaida na Wakatoliki waaminifu huilinda heshima hii katika kila nyanja ya maisha yao, ikiwa ni pamoja na shughuli zao kitaalamu. Wafanyakazi Katoliki katika huduma za afya, anaendelea kueleza, hutoa changamoto katika mifumo wa afya duniani iliyo kinyume na utetezi wa maisha katika asilia yake , hasa katika kutetea makundi ya wadhaifu , kama wale ambao bado kuzaliwa na wazee , kama imani yao inavyowataka.


Makala imeendelea kuangalisha katika ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisco,kwa Siku ya Wagonjwa ya Duniani 2015, ambamo ameonye juu ya uongo unaofanyika kwa kutumia mgongo wa ufanikisha huduma bora katika makundi ya kijamii lakini ukweli wake halisi ni kuangamiza maisha ya watu dhaifu wasioweza kujitetea wenyewe kwa ushupavu, mfano watoto wachanga wasiozaliwa bado, wagonjwa mahututi wasiojiweza wanao chaguliwa matibabu ya eutanasia , au maisha ya wazee yanayokatishwa kwa kunyimwa huduma, kutokana na uzee wao. Na pia hata wale wanaojaribu kutetea maisha ya watu hao, sauti yao hunyamazishwa kwa vitisho vya kufutwa katika upeo wa huduma za afya za kijamii.
Huku ni kunyamasisha sauti ya imani katika huduma za afya .

Makala inaendelea kusema, bila imani katika huduma za afya, nani ataweka breki kwa makampuni ya dawa yanayotafuta kutengeneza dawa kwa manufaa yao binafsi? Wapo wengi wanaotaka kutengeneza dawa kwa lengo la kuvuna utajiri bila kujali athari za maisha ya wengine.

Na Madaktari , Franklin Miller na Robert Truog, wanasema, bila kuzingatia maadili ya kidini ni nani atakuwa mtetezi wa maisha hadi kifo chake cha kawaida? Ni nani atakayekemea uvunaji wa viungo muhimu kutoka kwa watu wengine na hasa walio wanyeonge katika jamii? Ni nani atakaye simama dhidi ya mmomonyoko wa uhuru wa kidini katika huduma za afya na zaidi ya vishio katika fani ya Maisha ya Katoliki katika huduma ya afya?. Hakuna isipokuwa ni misingi ya maadili ya imani, kulindwa na kutambuliwa kama ni haki msingi katika nguvu ya kutetea heshima na haki za watu binafsi dhidi ya urasimu tenge katika mizania ya heshima ya maisha ya mtu.

Makala imehimiza walio katika uwanja huu wa huduma za afya na hasa watalaam na wahudumu , kuuanza mwaka huu kwa kufanya kazi kwa bidii zaidi hasa katika kupambana na wimbi la unyanyasaji wa imani ya kidini katika huduma ya afya. Lazima dhamiri za kidini zilindwe na kutetewa na wataalam wote wa afya.








All the contents on this site are copyrighted ©.