Wamissionari wawili waliokuwa wametekwa nyara na watu wenye silaha huko Jamhuri ya
Watu wa Afrika ya Kati, hivi karibuni, hatimaye, wameachiwa huru. Serikali ya Ufaransa
imempongeza kwa namna ya pekee, Askofu mkuu Diedonnè Nzapailanga wa Jimbo kuu la Bangui,
kwa jitihada zake ambazo zimewezesha wamissionari hao kutoka Ufaransa kuweza kuachiliwa
huru.
Kwa sasa kuna juhudi zinazoendelea za kutaka kumwokoa Jenerali Andjilo
aliyekuwa anaongoza kampeni dhidi ya Kikundi cha Balaka, aliyekamatwa tarehe 18 Januari
2015 na Vikosi vya Umoja wa Mataifa, vinavyofanya kazi huko Afrika ya Kati.